Quantcast
Channel: Gospel Kitaa™
Viewing all 1245 articles
Browse latest View live

SOMO: SIRI YA KIFO CHA GHAFLA (KUCHUKULIWA MSUKULE) - ASKOFU GWAJIMA

$
0
0

SOMO: Siri ya kifo cha ghafla (Kuchukuliwa msukule)

Imeandikwa: Mambo ya walawi 19:26 "Msile kitu cho chote pamoja na damu yake; wala msifanye kuloga, wala kutumia utambuzi."
Imeandikwa: Kumbukumbu la torati18:10-11"Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, wala mtu awaombaye wafu."


Kwenye Biblia imeonyesha mtu anaweza akalogwa na wachawi wapo.

Imeandikwa: Wagalatia 3:1 "Enyi Wagalatia msio na akili, ni nani aliyewaloga, ninyi ambao Yesu Kristo aliwekwa wazi mbele ya macho yenu ya kuwa amesulibiwa?"

Inamaanisha kuna mambo mtu anaweza akayafanya ikiwa tu amelogwa na wachawi. Mtu anaweza akawa amekufa kichawi kabisa na wachawi ndio wanaokuwa wamemchukua na kumfanya msukule. Huku duniani tunaweza tukawa tunafahamu fulani amefariki kumbe ameibiwa yupo mahali anafanya kazi fulani na nyota yake inatumika huko.

Wafalme wengi duniani wamejengwa na uchawi.

Imeandikwa: Danieli2: 1 "Hata katika mwaka wa pili wa kumiliki kwake Nebukadreza, Nebukadreza aliota ndoto; na roho yake ikafadhaika, usingizi wake ukamwacha. Ndipo mfalme akatoa amri kuwaita waganga, na wachawi, na wasihiri, na Wakaldayo, wapate kumweleza mfalme ndoto zake. Basi wakaingia, wakasimama mbele ya mfalme. Mfalme akawaambia, Nimeota ndoto, na roho yangu imefadhaika hata niijue tafsiri yake."

Mfalme Nebkadreza aliishi miaka zaidi ya mia sita kabla ya kuzaliwa kristo. Alikuwa amejenga utawala wake kwa kutegemea waganga wa kienyeji na wachawi.

Imeandikwa: Kutoka 7: 11 "Ndipo Farao naye akawaita wenye akili na wachawi; na hao waganga wa Misri wakafanya vivyo kwa uganga wao."

Imeandikwa: Danieli 5:7 "Mfalme akalia kwa sauti kubwa, akaamuru waletwe wachawi, na Wakaldayo na wanajimu. Mfalme akanena, akawaambia wenye hekima wa Babeli, mtu awaye yote atakayesoma maandiko haya, na kunionyesha tafsiri yake, atavikwa mavazi ya rangi ya zambarau, na kuwa na mkufu wa dhahabu shingoni mwake, naye atakuwa mtu wa tatu katika ufalme."

Mfalme Nebkadreza, Farao na Mfalme wa Babeli wote hawa walikuwa wanatumia uchawi kwenye tawala zao.

Kuna wachawi wanafanya vitu kwa ruhusa ya wafalme wa nchi. Ukiwa na Bwana Yesu ndani yako unakuwa huwezi kulogwa wala kuonewa na shetani na mawakala wake.

Wokovu sio dini wala dhehebu wala ulokole, wokovu ni kuingia ndani ya Ufalme wa Yesu na kutua mizigo yako sababu amesema njooni kwangu ninyi nyote mlemewao na mizigo nami nitawapumzisha. ukiwa na Yesu huwezi kulogwa iwe ni kwenye chakula, kwenye gari, kwenye kinywaji, kazini, kwenye biashara au mahala popote sababu unakuwa unaishi ndani ya Ufalme wa Mungu na unakuwa umezaliwa upya na kuwa mwana wa Mungu, kila kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu.

Imeandikwa: Hesabu 23:23 "Hakika hapana uchawi juu ya Yakobo, Wala hapana uganga juu ya Israeli. Sasa habari za Yakobo na Israeli zitasemwa, Ni mambo gani aliyoyatenda Mungu!"

Duniani kuna biashara ya kuuza wanadamu ambao husafirishwa kwenda nchi mbalimbali, kwenye ulimwengu wa rohoni pia kuna biashara ya kuuza wanadamu inafanyika pia.

Imeandikwa: Nahumu 3:4 "Kwa sababu ya wingi wa ukahaba wa yule kahaba mzuri, yule bibi wa mambo ya uchawi, auzaye mataifa kwa ukahaba wake, na jamaa za watu kwa uchawi wake."

Taifa linaweza likauzwa likawa mali ya kuzimu, mapato yote yanayopatikana unakuwa huoni yanakwenda wapi.

Imeandikwa: Ufunuo 18: 11 "Nao wafanya biashara wa nchi walia na kumwombolezea, kwa sababu hapana mtu anunuaye bidhaa yao tena; bidhaa ya dhahabu, na fedha, na kito chenye thamani, na lulu, na kitani nzuri, na nguo ya rangi ya zambarau, na hariri, na nguo nyekundu; na kila mti wa uudi, na kila chombo cha pembe, na kila chombo cha mti wa thamani nyingi, na cha shaba, na cha chuma, na cha marimari; na mdalasini, na iliki, na uvumba, na marhamu, na ubani, na mvinyo, na mafuta ya mzeituni, na unga mzuri, na ngano, na ng'ombe, na kondoo, na farasi, na magari, na miili na roho za wanadamu. Na matunda yaliyotamaniwa na roho yako yamekuondokea; na vitu vyote vilivyo laini na vitu vya fahari vimekupotea; wala watu hawataviona tena kamwe."

Watu wanawinda roho za watu na kuziuza kama bidhaa kwa wafanya biashara. Mungu anasema atazitoa roho hizo mikononi mwao walioziiba kwa nguvu na kuzirudisha kwa watu.

Imeandikwa: Ezekiel 13: 20 "Basi Bwana MUNGU asema hivi; Tazama, mimi ni kinyume cha hirizi zenu, ambazo kwa hizo mnaziwinda roho za watu kama ndege, nami nitazitoa katika mikono yenu kwa nguvu; nami nitaziachilia roho zile mnazoziwinda kama ndege.

Wachawi wanaweza wakaiba miili na roho za watu na pia wanaweza wakaiba viungo vya mtu kama moyo, akili, nyota, mikono kwenye ulimwengu wa rohoni huku mtu aliyeibiwa akiwa na mgonjwa mara kwa mara na kuwa na mikosi au wanaweza wakamchukua mtu mzima mzima na kumtumikisha kwa shughuli zao za kichawi huku akidhaniwa kwamba amekufa.

Imeandikwa: Isaya 42: 22 "Lakini watu hawa ni watu walioibiwa na kutekwa; wote wamenaswa katika mashimo, wamefichwa katika magereza; wamekuwa mawindo, wala hapana aokoaye; wamekuwa mateka, wala hapana asemaye, Rudisha."

Mtu anaweza akaibiwa na kuuzwa, Yuda alimuuza Yesu kwenye ulimwengu wa mwili lakini kwenye ulimwengu wa rohoni mtu anaweza akaibiwa akaoneka amefariki kumbe ameibiwa na kupelekwa kutumikishwa mahali kufanya kazi fulani.

Imeandikwa: Mathayo 10: 7 "Na katika kuenenda kwenu, hubirini, mkisema, Ufalme wa mbinguni umekaribia. Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure."

Unaweza ukawa unaishi na mtu haeleweki kitabia au kiakili kumbe mtu huyo kiroho ameibiwa na anatumikishwa mahali na huyo uliye naye siyo yeye halisi unaye mfahamu. Mtu mwingine anaweza akawa amapatwa na ajali anakufa papo hapo lakini kuihalisia anakuwa hajafa ila amechukuliwa msukule na kupelekwa sehemu ili afanyishwe kazi.

Au mtu anaweza akawa amelala usingizi akafariki akiwa amelala , mtu huyu anakuwa ameibiwa msukule na mara nyingi watu wa nanaofariki namna hii huwa wanazikwa siku hiyohiyo ili iwe rahisi kuchukuliwa msukule wasije akarudishwa. Watu wa aina kama hizo ndio wanaitwa wameibiwa.

BAADA YA MAOMBI YA KUWARUDISHA WATU WALIOIBIWA NA KUTEKWA KULIKUWA NA SHUHUDA NYINGI LAKINI BAADHI YA SHUHUDA HIZO NI.

Dada mmoja ambaye amerudishwa ameeleza alikuwa anatumikishwa kwenye shughuli za kubeba mizigo na kufua nguo za watu pamoja na kulima na mkoani Morogoro. Alikuwa pamoja na watu wengi waliochukuliwa msukule. Anaeleza kwamba alisikia sauti ya watu wengi ikimuita njoo na ghafla akajikuta yupo kanisani na kuona watu wengi. Amemshukuru Mungu kwa kumwokoa na kuahidi kumtumikia maisha yake yote.

Dada mwingine ambaye amerudishwa ameeleza kwamba alikuwa amechukuliwa na Babu yake alifariki siku nyingi tangu akiwa mdogo ambaye alitaka amfanye malkia ili azae watoto wa kijini. Dada huyo ameelezea kwamba akiwa chini ya bahari alilishwa pete mbili na Babu yake ili akiwa mtu mzima azae watoto kutokana na pete hizo, ameelezea wakati akiwa huko kuzimu alisikia watu wakiita Njooo ndipo akaambiwa mwili wamke umeenda sehemu ambayo siyo na akawaona watu wawili weupe wenye mabawa anamfuata na kumchukua na ghafla akajikuta yupo kanisani. Amemshukuru Bwana Yesu kwa kumwokoa na kuamua kumtumikia maisha yake yote.

MAOMBI NA SHUHUDA ZOTE ZA WATU WALIORUDISHWA MSUKULE ZINAPATIKANA KWENYE DVD.


ANGALIA PICHA ZA KINACHOENDELEA JIJINI MBEYA MSIBA WA MAMA YAKE BAHATI BUKUKU

$
0
0
Zifuatazo ni baadhi ya picha ya kile kinachoendelea katika msiba wa mama mzazi wa mwimbaji nyota wa muziki wa injili nchini Bahati Bukuku, huko jijini Mbeya. Kwa mujibu wa taarifa ambazo GK imezipata ni kwamba mwili wa marehemu umeshachukuliwa kutoka katika chumba cha kuhifadhia maiti hospitali ya rufaa jijini Mbeya.

Shughuli nzima za kuuaga mwili huo zinatarajiwa kufanyika nyumbani maeneo ya sinde mkabala na kihumbe jijini humo kisha maziko yatafanyika katika makaburi ya James. Mpaka sasa waimbaji mbalimbali wa muziki wa injili wamefika kumpa pole mwimbaji mwenzao akiwemo Boniface Mwaitege ambaye amekuwa karibu na Bahati Bukuku
















HATIMAYE KANISA ANGLIKANA LASEMA NDOA NI YA MKE NA MUME TU

$
0
0
Askofu mkuu kanisa Anglikana duniani, Justin Welby©belfasttelegrap

Kanisa la Kianglikana duniani limesisitiza kwamba ndoa ni kati ya mwanamume na mwanamke na likasimamisha ushirika wa jimbo la Marekani lililotambua ndoa za wapenzi wa jinsia moja.

Jimbo hilo la Marekani, ambalo kwa Kiingereza hujiita Episcopal Church, sasa halitaruhusiwa kushiriki kikamilifu katika masuala ya kanisa hilo.

Viongozi wa kanisa la Kianglikana duniani, waliokutana Canterbury, wamesema kanisa hilo lilikiuka Imani inayofuata na waumini wengi wa kanisa la Kianglikana kuhusu ndoa.

Marufuku hiyo ya muda ambayo imepewa jimbo hilo a Marekani inalenga kuzuia kugawanyika kabisa kwa kanisa hilo kutokana na tofauti kuhusu ndoa za wapenzi wa jinsia moja.

Ndoa hizo zimekuwa zikipingwa sana na majimbo ya kanisa hilo barani Afrika.

Uamuzi wa kusimamisha uanachama wa jimbo hilo la Marekani ulifanywa katika mkutano ambao umeeleza kuwa "mkali sana".

Askofu wa sasa wa jimbo hilo la Marekani Michael Curry amesema uamuzi huo "utasababisha uchungu mwingi". Mzozo kuhusu ndoa za jinsia moja ulianza kutokota baada ya kutawazwa kwa Kasisi Gene Robinson, aliyekuwa ametangaza hadharani kuwa mpenzi wa jinsia moja, kuwa askofu wa dayosisi ya New Hampshire ya jimbo hilo la Marekani mwaka 2003. Hatua hiyo ilizua mgawanyiko mkubwa miongoni mwa viongozi na waumini wa kanisa hilo duniani.


HABARI: DAKIKA CHACHE ZIMESALIA KUANZA KWA CAMPUS NIGHT, MAANDALIZI NI HIVI

$
0
0
Jukwaa limefungwa, taa ziko sawia kumulika kinachomulikika. Na haya ni sehemu tu ya maandalizi ya Campus Night ambapo dakika chache zijazo pale Sheikh Amri Abeid Karume Arusha ndio itakuwa mahala pa kukutana.

Usipange kukosa, Team GK ittakuwepo kukuletea tukio zima la usiku huu.
  


 spika zitakazotumika na hapo sipo katika mpangilio tayari kwa usiku huu
 fundi mitambo akiweka mitambo yake sawa
 Na huu ndio munekano mwa jukwaa kwa upande wa nyuma














VITUO VYA YATIMA VYALIOMBEA TAMASHA LA PASAKA 2016

$
0
0
Na Mwandishi Wetu
Sehemu ya misaada ambayo hutolewa na kampuni ya Msama Promotions.
Vituo mbalimbali vya kulelea watoto yatima jijini Dar es Salaam vinaliombea Tamasha la Pasaka 2016 kwa sababu Kampuni waaandaaji wa tamasha hilo mara zote huwakumbuka na kuwajali yatima.

Mmiliki wa kitupo cha Mandaliwa kilichopo Bunju, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, Halima Ramadhani alitumia fursa hiyo kumuombea Mungu muandaaji wa tamasha hilo, Alex Msama kuliendeleza tamasha hilo na amfungulie njia kila anachokifanya.

Ramadhani alisema Mungu amlinde na fitna za watu ili afanikiwe kwa sababu yatima wanalitegemea sana tamasha hilo ambalo linawasaidia mahitaji mbalimbali.

Mmiliki wa kituo cha Honoratha kilichopo Temeke, Honoratha Michael aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kumsaidia Msama katika kufanikisha tamasha hilo kwa sababu mojawapo ya vipaumbele vya Msama ni kuwasaidia yatima.

Katibu wa kituo cha Maunga kilichopo Kinondoni Moscow, Rashid Mpinda, anamshukuru Mungu kwa ajili ya Msama kusaidia yatima, na kwamba serikali imsaidie eneo ambalo litakuwa ni muunganiko baina ya yatima na jamii.

“Msama hana utajiri wowote, nawaomba wadau wengine wajitokeze kufanikisha misaada kwa jamii,” alisema Mpinda.

Aidha Mpinda alisema kila kituo chake wanamuombea dua maalum Msama kwa lengo la kufanikisha matakwa ya wenye uhitaji maalum.

Sudi Said wa kituo cha Zaidia kilichopo Sinza Madukani anazidi kuliombea Tamasha la Pasaka kwa sababu linawasaidia hivyo wako pamoja naye katika kufanikisha tamasha hilo.

EE BWANA NINA SHAUKU NDIO CHAGUO LA GK KUTOKA DINA MGOMERA

$
0
0


Mchana wa leo katika kanisa la TAG Ilala jijini Dar es salaam kunafanyika uzinduzi mkubwa wa DVD ya mwimbaji Dina Mgomera iitwayo 'Nina Haja Nawe' ambayo imerekodiwa katika viwango vizuri vya kukubariki wewe mdau na mpenzi wa muziki wa injili nchini.

Kutoka kwa mwanadada huyu tumekuchagulia wimbo wake kama chaguo letu kwako kwa jumapili ya leo wimbo unaitwa 'Ee Bwana' ni wimbo mzuri ambao tunaamini utakubariki. Kumbuka kufika katika kanisa la TAG Ilala ambalo lipo maeneo ya Kigogo sambusa ama mbele ya shule ya msingi Msimbazi Mseto kituo cha kushukia ni msimbazi centre. Barikiwa



TANZIA: MWIMBAJI NYOTA WA MUZIKI WA INJILI NCHINI CONGO AFARIKI DUNIA

$
0
0

Habari ambazo GK imezipata ni kwamba mwimbaji nyota wa muziki wa injili kutoka jamhuri ya Kidemokrasia  Kongo aitwaye Marie Misamu ametwaliwa kutoka dunia hii usiku wa kuamkia leo.

Taarifa za awali zinasema mwimbaji huyo aliyetokea kupendwa nchini humo na hata baadhi ya kazi zake kupatikana nchini Tanzania, alikuwa mgonjwa na kulikuwepo na ombi kutoka kwa bintiye aitwaye Ruth Misamu aliyewataka watu waliokuwa wakiulizia hali ya mwimbaji huyo kuwaomba wamuombee mama yake. Tutakujulisha endapo tutapata taarifa zaidi juu ya kifo chake

                Angalia kati ya kazi za marehemu zinazopatikana Tanzania. (Ee Yahwe)


             BWANA ALITOA NA BWANA AMETWAA JINA LA BWANA LIBARIKIWE

T.A.G ILALA KUMEPAMBA MOTO KATIKA UZINDUZI WA DVD YA DINA MGOMERA

$
0
0
Leo ni leo, asemaye kesho bado amelala, kwa maana milango ya baraka imeshafunguliwa pale kanisa la Tanzania Assemblies of God Ilala, ambapo Dina Mgomera anazindua DVD yake ye Nina Haja Nawe.

Kabla hata ya saa nane kutimu, makundi ya watu tayari yalikuwa eneo la tukio wakisikilizia tu muda rasmi, huku sauti ya kujaribu usikivu wa vyombo ndio zikipenya masikioni mwao na kuwa tulizo la roho.

Gospel Kitaa ambayo iko eneo la tukio, imeshuhudia nyuso zenye furaha, huku waimbaji kadha wa kadha wakiwa tayari kumrudishia Mungu sifa na utukufu kupitia uimbaji wa kutumia vyombo (live).
Sehemu ya watakaoimba leo ni pamoja na The Jordan Band, One Voice Family International, Bwana Harusi Edson Zako Mwasabwite (bofya kuona harusi yake), na wengine wengi.

Zifuatazo ni picha za awali wakati tamasha likiwa linakaribia kuanza. ambatana nasi.












Furaha Isaya

Kama bado hujajua kinachoendelea basi tazama video ifuatayo;




HATIMAYE MCHUNGAJI SAEED ABEIDINI AACHIWA HURU TOKA GEREZANI

$
0
0
Mchungaji Saeed Abeidini©ACLJ

Hatimaye Mungu amejibu maombi ya wakristo wengi waliochukua muda kumuombea mchungaji Saeed Abedini baada ya kuachiwa huru toka gerezani nchini Iran ambako aliwekwa kizuizini kwa kosa la kuhubiri injili nchini humo miaka takribani minne iliyopita.

Mchungaji Saeed ambaye ni raia wa Marekani lakini mzaliwa wa Iran aliachiwa huru siku ya jumamosi iliyoisha, baada ya kuwepo shinikizo kubwa kutoka kwa serikali ya Marekani, taasisi za haki za binadamu bila kusahau wakristo wakiitaka serikali ya Iran kumwachia huru mchungaji huyo. Ambapo taarifa zinasema mchungaji Abedini aliachiwa huru sambamba na wamarekani wengine watatu ambao nao walifungwa nchini humo.

Kwa upande wa mke wa mchungaji huyo aitwaye Naghmeh ambaye aliongoza kampeni mbalimbali za kuachiwa kwa mumewe bila kuchoka ikiwemo kuongoza maombi ya kufunga, katika tamko lake amesema kuachiwa kwa mumewe ni maombi kujibiwa, na kusema familia iko katika hali ya shukrani na kuwashukuru mamilioni ya watu walioshiriki nao katika maombi katika kuhakikisha mpendwa wao anaachiwa huru, aidha amesema kwasasa wanasubiri mchungaji huyo arudi kujiunga na familia yake. Aidha kuachiwa kwa mchungaji huyo kumekwenda sambamba na makubaliano kati ya serikali hizo mbili kuhusu kuachiwa kwa raia wa Iran waliokuwa kifungoni Marekani vivyo hivyo kwa raia hao wanne akiwemo mchungaji pia kuachiwa huru na Irani.

Mchungaji Saeed Abeidini ambaye alibadili dini kutoka uislamu na kuwa mkristo ni baba wa watoto wawili alihukumiwa kifungo cha miaka nane gerezani kwa kosa la kuhataraisha hali ya usalama nchini Iran (ingawa imetafsiriwa kama kosa la kuhubiri na kutaka kubadilisha watu imani yao ya kiislamu ili wawe wakristo jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi hiyo ya kiislamu ya Iran). Ambapo wakati wa kukamatwa kwake alikuwa nchini humo akijenga kituo cha kusaidia watoto yatima. Familia yake imesema mchungaji Abeidini alifanyiwa mateso na manyanyaso gerezani ili aikatae imani yake mpya ya Kikristo lakini hakuogopa kusema na kusimamia ukweli juu ya Kristo.

KINANA ALITAKIA HERI TAMASHA LA PASAKA 2016

$
0
0
Ndugu Kinana ©DewjiBlog.
Na Mwandishi Wetu.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Abdulrahman Kinana amelitakia heri Tamasha la Pasaka la mwaka huu linaloandaliwa na Kampuni ya Msama Promotions.

Akizungumza mwishoni mwa wiki, ofisini kwake, Lumumba jijini Dar es Salaam, Kinana analitakia heri na fanaka tamasha hilo na kumuomba Mungu aendelee kubariki utulivu na mshikamano kwa Watanzania wote.

Kinana alisema Tamasha la Pasaka lengo lake ni ujenzi wa Taifa letu na kudumisha amani na utulivu tulionao sambamba na jukumu kubwa la kupiga vita umasikini na kuboresha maisha ya Watanzania na kufikia kiwango cha juu cha maendeleo.

Kinana alisema Watanzania tuna wajibu wa kudumisha mshikamano na upendo miongoni mwetu na tuendelee kusaidiana katika kila hali.

“Tamasha la Pasaka mwaka huu liwe ni muongozo wa kudumisha mshikamano na upendo miongoni mwetu ili tuendelee kusaidiana katika kila hali,” alisema Kinana.

Katibu huyo alisema Watanzania tunatakiwa kuzingatia hayo ili sote kuwa pamoja ili tupige hatua stahili na kuondokana na umasikini uliokithiri.

Mwisho

HOJA: BARAKA ZA KIUCHUMI ZIMEJENGWA JUU YA ARDHI

$
0
0
Askofu Sylvester Gamanywa,
WAPO Mission International.


Tumekuwa na utamaduni wa kuomba na kuamini kupokea Baraka za kiuchumi kutoka kwa Mungu kwa njia ya imani. Lakini tumejijenga upande mmoja na kusahau au kuacha upande wa pili ambao majibu ya maombi yetu hayawezi kuwa halisi kama tusipofanya maandalizi yake. Uchumi katika maana yake halisi hata kama unaanza kwa imani lakini lazima kilele chake ni kuonekana kwa macho. Na kuonekana kwa macho lazima kunahusisha ardhi:

Ardhi ndio msingi wa
Baraka za kiuchumi duniani

Maisha ya kila siku yanafanyikia duniani. Duniani maana yake kwenye ardhi. Kila kitu ulichonacho au shughuli unayofanya inategemea ardhi. Tumeamka pamoja alfajiri tukuwa wapi? Kwenye ardhi. Nyumba na chumba ulimolala leo kipo juu ya ardhi. Unapokwenda leo iwe shuleni, kazini, kwenye ujasiriamali popote ulipo unafanyikia kwenye ardhi.

Kama wewe huna ardhi unayomiliki inayohusiana na shughuli zako, unajua kabisa kwamba sehemu ya mapato yako itakuwa ni kulipia pango za nyumba kuanzia kuishi na sehemu ya biashara. Lakini kama unamiliki ardhi yako ambayo ina nyumba yako ya kuishi au shughulii yoyote ya uzalishaji au unapangisha utaiona ardhi ilikuwa ni sehemu ya mapato yako badala ya kuwa matumizi ya mapato yako.

Kana kwamba hii haitoshi, Yesu Kristo mwenyewe ameitaja ardhi na kuitumia katika mafundisho yake. Lakini zaidi pamoja na mafundisho yake pia aliagiza kufanyika kwa mabadiliko ya kimfumo kuhusu suala zima la uchumi na imani. Yesu aliweka vigezo vya kustahili kuwa wanafunzi wake akiwaamuru wampe yeye Nafasi ya kwanza mioyoni mwao kabla ya jamaa na vitu wanavyovithamini.

Katika Luka 14:26-27; Yesu Aliamuru yeye kuwa kwanza kabla ya wazazi, ndugu na jamaa katika familia.  Katika Luka 14:33; Yesu aliweka msimamo kwamba asiyeweza kumtaguliza Kristo kuliko jamaa na mali hafai kuwa mwanafunzi wake:

Lakini upande wa pili wa sarafu kuhusu mabadiliko ya kimfumo, Yesu alitoa ahadi kwa wale watakaokidhi vigezo vya kuwa wanafunzi wake kwamba kumpa Nafasi ya kwanza, hawatakuwa wakiwa au mafukara. Katika Mathayo 19:29 na Marko 10:29 Yesu anataja walioacha nyumba na mashamba watapata mali hizo mara mia katika ulimwengu huu wa sasa!

Ukitafakari Baraka za kiuchumii alizoamuru Yesu kwa wanafunzi wake zote zinahusiana na ardhi! Mashamba hulimwa kwenye ardhi na nyumba hujengwa kwenye ardhi. Ujumbe wa leo ni kwamba maandalizi ya Baraka zako za kiuchumi lazima yaanze na kumiliki kipannde cha ardhi. Hii ni wajibu wako na haihitaji muujiza.

Kuna mambo Yesu alisema tuombe lakini kuna vingine alisema tutafute. Kimojawapo cha kutafuta ni Ardhi. Kama unacho kipande tayari, basi ongeza kingine. Kama hauna anza sasa kutafuta mpaka upate. Ni muhimu kwa Baraka zako za kiuchumi.

Jinsi mitume walivyotekeleza
mchakato wa uchumi na imani

Maagizo mengi yaliyotolewa na Yesu, Mitume wake walianza kuyatekeleza tangu siku ya Pentekoste pale aliposhuka Roho Mtakatifu. Moja wapo ya utaratibu wa utekelezaji wa maagizo ya Yesu ni kujenga mifumo maalum. Mojawapo ya mifumo hiyo ni “MFUMO WA VIKUNDI VYA NYUMBA KWA NYUMBA.”

“Na siku zote kwa moyo mmoja walidumu ndani ya hekalu, wakimega mkate nyumba kwa nyumba, na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe,…” (Mdo.2:46)

Huu ulikuwa ni mfumo ambao uliwafanya maelfu ya  waamini kujenga uhusiano wa karibu na Mungu lakini pia uhusiano wa karibu miongoni mwao.

Kila kikundi kilikuwa na nyumba ambayo ilitumika kwa ajili ya mikutano yote kuanzia ibada, maombi, mpaka masuala ya kijamii na kiuchumi. HAWAKUTENGANISHA IMANI NA UCHUMI. Ndiyo maana utakuta imeandikwa waziwazi kwamba, mali zao za viwanja, nyumba na mashamba vilitumika katika kuwezeshana kiuchumi, na hivi ndivyo walivyotekeleza maagizo waliyokabidhia na Yesu:

“Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vilivyouzwa, wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadri alivyohitaji.” (Mdo.4:34)

“Na Yusufu aliyeitwa na mitume Barnaba (maana yake, Mwana wa faraja) Mlawi, asili yake ni mtu wa Kipro, alikuwa na shamba akaliuza, akaileta fedha, akaiweka miguuni pa mitume.” (Mdo.4:36-37)

Mpendwa msomaji, hapa tunasoma habari za kanisa la kwanza la mitume ambalo Yesu alitabiri kwamba atalijenga na milango ya kuzima haitalishinda. Mitume walijenga msingi wa uchumi endelevu ambao ulitegemea mtandao wa vikundi vya nyumba kwa nyumba na huduma za kiroho na kiuchumi vyote vilienda sambamba.

Changamoto za kanisa
la leo na ufumbuzi wake

Tumeshajionea kwamba Yesu Kristo aliwaachia wanafunzi wake mabadiliko ya kimfumo kwa habari za uchumi na imani akitaka kipaumbele kiwe ni Yeye kwanza na familia na mali vishike nafasi ya pili. Pili, alitoa ahadi ya Baraka za kiuchumi ambazo alitamka waziwazi kuwa watafanikiwa kiuchimi mara mia

Piatumejifunza jinsi ambavyo mitume wa Kristo walivyoyatekeleza mabadiliko ya kimfumo kuhusu uchumi na imani kwa kujenga mfumo wa mtandao wa vikundi vya nyumba kwa nyumba ambamo masuala ya uchumi na imani vilisimamiwa kikamilifu na matokeo yake kanisa la kwanza lilikuwa na kuongozeka kiimani, kiroho na kiuchumi hata likawa tishio kwa madhehebu ya dini ya kiyahudi yaliyokuwepo kabla yake.

“Wala hapakuwa na mtu mmoja miongoni mwao mwenye mahitaji; kwa sababu watu wote waliokuwa na viwanja au nyumba waliviuza, wakaileta thamani ya vitu vilivyouzwa, wakaiweka miguuni pa mitume; kila mtu akagawiwa kwa kadri alivyohitaji.” (Mdo.4:34)

“Na kwa mikono ya mitume zikafanyika isharaa na maajabu mengi katika watu; ….na katika wote wengine hapana hata mmoja aliyethubutu kuambatana nao; ila watu waliwaadhimisha; waliaomini wakazidi kuongezeka kwa Bwana, wengi, wanaue na wanawake…” (Mdo.5:12-14)
Tatizo kubwa la kanisa la leo ni dhana potofu ya kutenganisha Uchumi na Imani. Tafsiri ya jumla ni kutafsiri kwamba mambo ya uchumi ni ya kidunia na kimwili na Imani ni mambo ya kiroho ambayo yanajitegemea na hayatakiwi kuchanganywa na mambo ya uchumi. Ikiwa Yesu na Mitume wake hawakutenganisha uchumi na imani, sisi tumeipata wapi hii dhana ya kutenganisha uchumi na imani?

Athari za “kutenganisha uchumi na imani” ni pamoja na kuwafanya waamini wakiuke kanuni za unafunzi kwa Kristo ambaye aliagiza kushika nafasi ya kwanza kuliko vyote: Waamini wakitenganisha uchumi na imani, wanageuka kuwa ndio wamiliki wa uchumi na waamuzi wa mwisho badala ya Kristo. Tayari kwa mujibu wa Yesu wanapoteza sifa ya kwa wanafunzi wake

Athari ya pili ya “kutenganisha uchumi na imani” waamini hawawezi kukua kiimani kwa sababu muda mwingi wanautumia kwenye uchumi tangu asubuhi hadi jioni, jumatatu mpaka Jumamosi. Na shughuli wanazozifanya hazijajengwa kwenye maadili ya kiimani kwa hiyo wanaishi maisha ya mchanganyo.

Athari ya tatu inaliathiri kanisa kihuduma kwa kushindwa kuhubiri injili kwa upana kwa sababu halina nguvu za kiuchumi. Linaendesha huduma zake kutegemea matoleo ya waamini ambao naoo hawatoi kwa viwango kwa sababu wametenganisha uchumi na imani. Mpaka mara nyingine uongozi unalazimika ama kutumia vitisho vya matoleo au kutumia ulaghai kwa kuwaahidi watu kubarikiwa kwa kutoa lakini Baraka zenye hazionekani kama zinavyoahidiwa. Matokeo yake waamini wanapoteza imani na kurudi nyuma.

Ufumbuzi ulioko sasa, ni kurejea kwenye misingi ya iliyojengwa na mitume wa kanisa la kwanza. Kanisa lazima libebe jukumu la kuelimisha na kuhamasisha na hata kuwezesha waamini wake kumililiki ardhi na kuitumia kwa njia za uzalishaji wa mitandao ya vikundi kama ilivyokuwa katika kanisa la kwanza.

Vikundi vya kiuchumi vikianzishwa wajibu wa kanisa ni kufundisha maadili ya kiimani na kuhakikisha sehemu ya mapato inakuja kwenye huduma za kiinjili kama kanisa la kwanza. Hapo ndipo Injili itahubiriwa kwa kishindo, na waamini watainuka kiuchumi, na jamii itajua kuwa hili ndilo kanisa la Kristo Mfalme wa wafalme mbinguni na duniani.  

(mwisho)

KANISA ASSEMBLIES OF GOD LAZIDI KUMEREMETA KWA MAENDELEO

$
0
0

Uzinduzi wa bweni la kisasa la wanaume - chuo cha Biblia (Central Bible College) -Dodoma

Idara ya Elimu ya kanisa la Tanzania Assemblies of God linatekeleza mpango wa maboresho wa vyuo vyake vya Biblia nchi nzima. Mwezi Januari Mwaka 2016, jengo jipya lenye uwezo wa kuchukua wanafunzi wanaume zaidi ya 200 katika chuo cha Biblia cha Central Bible College (CBC) Dodoma lilizinduliwa katika hafla iliyoongozwa na Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies of God Rev. Dr. Barnabas Mtokambali. Mradi huu umefadhiliwa kwa ubia baina ya "Priority One"kutoka Marekani na Idara ya Elimu ya TAG.

Akizungumza katika uzinduzi huo, Mgeni Rasmi Dr. Sam Johnson kutoka Marekani ambaye pia ndiye mfadhili mkuu wa mradi huo alisema mradi huo ni utekelezaji wa Agizo Kuu la Bwana Yesu la kuwafanya mataifa yote kuwa wanafunzi wa Yesu. Dr. Johnson alisema chuo cha CBC kitawavutia watumishi wengi kuja kunolewa na kupata elimu ya theolojia ili waje kuwa watumishi wazuri zaidi, kwa kupata Stashahada, Shahada, na Shahada za Uzamili na Uzamivu. Aliongeza kwamba anaamini kwamba CBC itakuwa kitovu cha umahiri katika elimu ya theolojia hapa Tanzania na nje ya Tanzania.

Kwa upande wake Askofu Mkuu wa Tanzania Assemblies of God, Rev. DR. Mtokambali alisema anapolitazama jengo hili na aliposikia historia yake kutoka kwa Mkurugenzi wa Elimu, anaona mbali zaidi ya mamilioni ya shillingi yaliyotumika. Alisema anaona mamilioni ya roho za watanzania na wasio watanzania zikiokolewa kupitia elimu itakayotolewa katika chuo hiki. Alisema katika Mpango Mkakati tumefanya kazi nzuri miaka saba iliyopita na kwamba miaka mitatu iliyobaki ni ya kufanya kazi ya kufa na kupona ili tuivune Tanzania kwa ajili ya Yesu.

Askofu mkuu alimshukuru Dr. Sam Johnson na "Priority One" kwa ukarimu wao wa utoaji, Mkurugenzi wa Elimu Rev. Jonas Mkoba kwa kujitoa kwakwe kusimamia mradi huu, na kila mtu aliyeshiriki kwa njia moja au nyingine kuukamilisha mradi huu. 

Taarifa kwa mujibu wa tovuti ya kanisa hilo Tanzania Assemblies of God 

Angalia picha za tukio la uzinduzi kwahisani ya TAG 


















MAKALA: KAZI YA USAMBAZAJI NA VILIO VYAKE

$
0
0
John Maulid,
GK Staff writer.

Nakala ya CD ©wikimedia

Kurekodi nyimbo yaweza kuwa kitu chepesi, na hata kurekodi video pia. Lakini shughuli huanza hasa pale unapokuwa na kazi yako mkononi kisha hujui uanzie wapi ili iwafikie wapenzi wa muziki wa injili.

Kwa vilio hivi nimeguswa kuwashauri na pia kuwafungua wale waimbaji wasiojua chochote katika tasnia hii ya muziki wa injili hasa kuhusu kusambaziwa kazi zao. Waimbaji wengi wanalia na wasambazaji, kila mmoja analia kimpango wake; hii mimi inaniumiza kwakweli unakuta mtu ana nyimbo nzuri lakini inakataliwa lakini unakuta kuna mwingine ameimba “vibaya” albam yake ikachukuliwa. Wewe uliyekataliwa wala usijilaumu wala kujilaumu kwamba una mkosi.

Kuna kitu kinaitwa tamaa, na tamaa humshinda binadamu asiye na hofu ya Mungu.

Kuna watu wamepewa kibali cha kusikiliza kazi ya muimbaji kama ipo vizuri ipitishwe na kusambazwa. Sasa ile nafasi unakuta mtu anaitumia vibaya anataka umpe pesa ili kazi yako isambazwe. Kwa muimbaji asiye jiamini anakubali kutoa hongo halafu unakuta albam inafanya vizuri madukani lakini yeye mwenyewe hana chochote. Hicho ndicho kinachowaumiza waimbaji wengi.

Kingine, kazi nyingi zinaibiwa kutokana na mikataba feki inayofanywa; mathalani unaweza kusaini nakala elfu moja. Hivi kweli kopi elfu moja zinaweza kusambazwa hadi mikoani? Wakati dukani kwake kwenyewe tu unakuta hazitoshi.

Cha ajabu ni kwamba hizo kopi elfu moja Mji wa Dar, na ukienda mikoani napo kila kona nakala zipo. Kwa kweli huwezi Kufikia Malengo yako kwa namna hiyo, pale kazi nyingi zinapoibiwa na wasambazaji.

Kuna baadhi ya wasambazaji unakuta mnasainishana kopi kadhaa halafu hatoi tena na ukivunja nae mkataba unakuta bado anazitoa bila wewe kujua. Wapo wengi wanaofanya michezo ya namna hiyo; kupata msambazaji mwaminifu ni zoezi la kutoa jasho siku hizi. Unaweza kukuta kazi imefika hadi nchi za jirani, lakini imefikaje na wewe labda umesain mkataba wa hapa Tanzania tu.

Wengi hawajui labda niwafungue;

Unapoingia mkataba na msambazaji kuna mikataba miwili; wa ndani ya nchi yako na nchi nyingine, kwa hiyo kama mtasaini wa hapa Tanzania, basi haruhusiwi kuivusha kazi yako nchi nyingine ila wewe unaweza kwenda kuiuza tena labda Kenya au Uganda au nchi nyingine yoyote ile uipendayo.

Pia siku hizi kumezuka mfumo mpya eti kwamba kazi inapopelekwa kwa msambazaji Inabidi producer wa video ammegee yule anaeipitisha kazi Umpe asilimia kidogo ili isambazwe. Na kuna baadhi ya kampuni za kurekodi video zinakubali na kufanya hivyo.

Kikubwa cha kuwashauri waimbaji ni kujiamini na kutotegemea sana soko la Tanzania. Pia wakati nwingine fursa ya kuuza master ikipatikana, uza ili usihangaike na Msabazaji. Lakini pale unapouza master, basi tambua ya kwamba huna haki zozote tena za kuiuza hiyo kazi yako, umeshahamisha umiliki. Ikiendelea kuuza kwa kipindi cha miaka 50, hilo halitokuwa na faida kwako.

Katika haya yote, ni muhimu kumuomba Mungu akuwezeshe kufanya maamuzi sahihi, na hata kuwa na watu bora wa kuisambaza kazi yako. Haleluya!

SOMO: IMANI INAYOKUHAKIKSIHIA MAVUNO UTOAPO SADAKA YA MBEGU - MWL MWAKASEGE

$
0
0

Mwalimu - Christopher Mwakasege
Diamond Jubilee 17 Jjanuary 2016

SEMINA YA KUPANDA NA KUVUNA.


Bwana Yesu asifiwe , leo tunapo angalia somo hili nataka tuangalie sana IMANI ILETAYO MATOKEO
Msisitizo haupo katika sadaka bali kwenye ni kwenye Imani na msisitizo haupo kwenye kupanda na kuvuna bali upo kwenye Imani. Japo kuna watu huwa wanaambatanisha na maombi wanapotoa sadaka lakini bado msisitizo upo kwenye Imani.

Waebrania 11:31 ‘’ 31Kwa imani, Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.

Msisitizo hapa upo KWA IMANI. Na sio ukahaba au wale wapelelezi bali msisitizo hapa ni Imani. Na ndio maana biblia inaonesha matokeo ya Imani yake.

Yoshua 2:8-13  8Kabla wale wapelelezi hawajalala, Rahabu akawaendea huko juu darini, 9 akawaambia, “Ninajua kuwa BWANA amewapa nchi hii na hofu kuu imetuangukia kwa sababu yenu, kiasi kwamba wote waishio katika nchi hii wanayeyuka kwa hofu kwa sababu yenu.
10Tumesikia jinsi BWANA alivyokausha maji ya Bahari ya Shamua kwa ajili yenu mlipotoka Misri, pia lile mlilowatendea Sihoni na Ogu, wafalme wawili wa Waamori mashariki ya Yordani, ambao mliwaangamiza kabisa. 11Tuliposikia juu ya hili, mioyo yetu iliyeyuka na kila mmoja alikosa ujasiri kwa sababu yenu, kwa maana BWANA Mungu wenu ni Mungu aliye juu mbinguni na duniani chini. 12Sasa basi, tafadhali niapieni kwa BWANA, kwamba mtaitendea hisani jamaa ya baba yangu, kwa kuwa mimi nimewatendea hisani. Nipeni ishara ya uaminifu. 13kwamba mtayahifadhi maisha ya baba yangu na mama yangu, ndugu zangu wa kiume na wa kike, pamoja na wale wote walio wa kwao na kwamba mtatuokoa na kifo.’’

Hii habari tunajifunza sana Imani inapohakikishwa mavuno unapotoa sadaka ya mbegu. NA KUMBUKA HILI LITAKUSAIDIA, Imani ya Rahabu haikuwa kwenye sadaka au maombi au matendo ya kukaribisha wapepelezi balli ilikuwa kwenye matokeo ya Imani yake alipotoa ile sadaka.
Fahamu sana umuhimu wa Imani hizi unapotoa sadaka yako.


USIWEKE IMANI YAKO KWENYE SADAKA BALI WEKA IMANI YAKO KWA MUNGU.
Sadaka haisukumi jibu la Mungu Bali Mungu ndiye anayejibu. Na utaona mwingine ameweka Imani yake kwenye maombi na yasipojibiwa anapata shida sana. Ila kumbuka hili weka Imani yako kwa Mungu na yeye atakusaidia kwa kupitia Imani uliyoiweka kwake.

Waebrania 11:1 ‘’ Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya  mambo yasiyoonekana’’

Waebrania 11:6 ‘’ 6Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza Mungu, kwa maana ye yote anayemjia Mungu lazima aamini kwamba Yeye yuko na ya kuwa huwapa thawabu wale wamtafutao kwa bidii.

Warumi 10:17 ‘’Basi Imani chanzo chake ni kusikia na kusikia huja kwa neno la kristo.

Yakobo 2: 17,20 ‘’ Vivyo hivyo, imani peke yake kama haikuimbatana na matendo, imekufa, 20Je, wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani bila matendo haifai kitu?

ZINGATIA HAYA. IMANI BILA MATENDO IMEKUFA NA IMANI ISIPOKUWA NA MATENDO HAIZAI.
Sasa Twende tutafsiri ile KWA IMANI RAHABU YULE KAHABA.
Sasa Toa neno Imani, hapo na weka ile ya Waebrania 11;1 itasomeka hivi KWA KUWA NA UHAKIKA WA MAMBO YATARAJIWAYO , , Rahabu, yule kahaba, hakuangamizwa pamoja na wale waliomwasi Mungu, kwa kuwa aliwakaribisha wale wapelelezi.Weka na Waebrania 11:6 , endeleza itasomeka hivi KWA KUWA ALITAKA KUMPENDEZA MUNGU NA ALIAMINI YA KUWA HUYU MUNGU YUPO NA KWAMBA ANAVYOMTAFUTA ATAONEKANA KWAKE NA KUMPA THAWABU

IMANI INAYOKUHAKIKISHIA MAVUNO UTOAPO SADAKA YA MBEGU/KAMA MBEGU.

Msisitizo wa ujumbe wa leo haupo kwenye sadaka au mavuno au maombi yanayoambatana na sadaka bali upo katika imabi

Ebrania 11:31

Joshua 2:8-13

Mara nyingi tutoapo sadaka tunaweka imani yetu kwenye sadaka.

Au tunaweka Imani kwenye maombi.

Ebrania 11:1

Ebrania 11:6

Rumi 10:17

Yakobo 2:17-20

Imani huja kwa kusikia. Rahabu alikuwa na Imani na Mungu wa Israel(Rahabu hakuwa Myahudi) kwa uaminifu ambao Mungu aliuonesha kwake.

Rahabu alisikia habari za Israel na kuona.

Mbegu kazi yake kubwa ni kubeba future. Unapotoa sadaka ta mbegu weka imani yako kwa MUNGU na kwa uaminifu wake.

Imani ina tabia...unaweza ukawa nayo na isikusaidie.

Hatuwezi kifikia standard ya maisha MUNGU ayatakayo tuyaishi pasipo msaada wake.

MAENEO 5 YATAKAYOKUSAIDIA KUJENGA IMANI YAKO KUKAA MAHALI HUSIKA AU KUPATA IMANI KAMA HAIPO AU KUIRUDISHA IMANI ILIYOPOTEA.

1. kuitambua na kuipokea mbegu.

2 korintho 9:10,11

Mungu anatoa mbegu na anatoa na mkate. Mbegu kwa ajili ya kupanda na mkate kwa ahili ya kula.

Mfano: umepewa 20,000 unajuaje ipi ni mbegu na ipi ni mkate.

Kilichobadilisha nyumba ya Rahabu kutoka kiwa mkate na kuwa mbegu

Galatia 6:7

2 korintho 9:6

2. Kwanini MUNGU amekupa hicho ulichonacho ukitoe kama mbegu

2 korintho 9:10-12

Watu wengi tuna sababu zetu za kutoa sadaka ya mbegu na ni muhimu sana kumuuliza Mungu ni kwanini ametaka utoe mbegu. Sababu moja wapo ni kuongeza kiwango chako cha ukarimu.

Hukubaliki mbele za Bwana kwa usichonacho bali kwa kile ulochonacho.

Muulize Mungu kwanini anataka utoe sadaka kama mbegu na kwa ajili ya nin.

Mbegu ni kwa ajili ya wewe kupata kile kilichopotea

Hekima ya Biblia inasema fikiri kwa ajili ya kesho.

Sababu nyingine ni kukuandaa kwa ajili ya new season.

Mbegu ina season ya kuleta mavuno. Na kupalilia na kunyeshea maji. Maana yake kukazia lile neno likilotumika wakati wa kupanda mbegu.

3.kujua aina ya arthi au udongo wa kupanda hiyo mbegu

Luka 8:11-15

Mbegu ni neno la Mungu. Kama unepewa Hela ili iwe mbegu lazima iambatane na neno la MUNGU na isipoambatana na neno la MUNGU haiwi mbegu ni hela tu. Kupanda mbegu bila maombi utapanda sehemu isiyo sahihi na hutapata mavuno.

Hali ya ardhi/udongo haibadilishwi na hali ya

mbegu yako. Isipokuwa hali ya udongo/ardhi inabadilisha hali ya mbegu yako.

Mungu anapokuelekeza kutoa ana sababu yake.

Mugu peke yake ndio ukimpa mbegu anaweza kuiua na kuikuza tena na ikazaa matunda.

Mungu lazima aiue mbegu ili kuikuza mana mbegu isipokufa haiwezi kuzaa. Mbegu yoyote yenye thamani kwako;

a) unaweza ukaila

b) unaweza usiipande na kuiweka tu ukafurahia kuiona.

Ndio mana lazima MUNGU aiue kwanza mbegu ili kuiotesha tena.

Rahabu alitambua ya kuwa kuna msaada kwa MUNGU wa israel pamoja na kwamba hakuwa mkristo.

Badilisha IMANI yako kama Rahabu alivofanya kwa kubadilisha matumizi ya nyumba yake kutoka kuwa dangulo na kuwa sadaka. Rahabu alichukua risk kubwa ili kulinda IMANI yake juu ya MUNGU wa Israel.

Imani inakutunza na inakutoa na inakupa uvumilivu mpaka kufikia season ya mavuno. Neno linasema utavuna kwa wakati wake usipozimia Roho. Ukiona unachoka lichunguze like neno la IMANI.

Sadaka ni devine invitation ya MUNGU ili kutengeneza katika maisha yako...

Shukrani kwa dada yetu Josephine kwa kutuandalia dondoo hizi ili nawewe msomaji wetu ujifunze

BWANA HARUSI EDSON AKONGA MIOYO YA WADAU UZINDUZI WA DINA MGOMERA

$
0
0

Edson Zako Mwasabwite, kutoka ndani ya fungate moja kwa moja akatokea kwenye tamasha la uzinduzi wa albam ya Nina Haja Nawe, yake Dina Mgomera. Tukio la kupanda madhabahuni na kuimba wimbo wa kwa Neema tu, ambao ulitanguliwa na wimbo mwingine mpya, ulibariki umati wa watu, wasiochoka kumueleza Mungu kuwa yu mwema.

Kabla ya kuimba, alianza kwa kumshukuru Mungu kwa tukio la kupata mke, ambaye ni mwema, na kuwashukuru zaidi watu kwa kumpa sapoti kwenye tukio lake hilo la kiMungu. (bofya kuona picha za harusi)

Edson na Asley
Sanjari na hayo Edson aliomba wananchi kumsapoti kijana Asley, ambaye anachipukia kwenye tasnia ya muziki wa injili, huku akiwa na shauku ya kufanya kazi binafsi kama ailivyo kwa Edson.

KWA TAARIFA YAKO : MTOTO WA ASKOFU ANAYEVUMA KANISA JINGINE BAADA YA KUHAMA KWA WAZAZI WAKE

$
0
0
Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu








KWA TAARIFA YAKO hii leo tunakujulisha kwa ufupi kati ya watoto wa watumishi waliobarikiwa vipaji mbalimbali hususani muziki lakini licha ya baraka za vipawa walivyonavyo, hawavitumii kwenye huduma za wazazi wao badala yake wanavuma sehemu nyingine. Mmoja kati ya watoto hao ambao hata hivyo kwa upande wake alipata ruhusa na uhuru kutoka kwa wazazi wake ni kijana aitwaye Freddy Washington Junior ambaye ni kiongozi wa sifa, mwalimu, mtunzi wa nyimbo, mpigaji wa takribani vyombo vya aina zote akitumika katika kwaya maarufu yenye tuzo kemkem duniani ya The Brooklyn Tabernacle ya jijini New York nchini Marekani.

KWA TAARIFA YAKO Freddy ni mtoto wa askofu Freddy Washington (wana majina sawa ila yeye mtoto anaitwa junior) ambaye licha ya kuwa ni askofu pia anasifa ya kuwa mwimbaji na mpigaji mzuri sana wa vyombo ujuzi ambao hapana shaka amemrithisha kijana wake ambaye pia amesomea masuala ya muziki katika moja ya vyuo hapo jijini New York Marekani. Wazazi wake Freddy wanaendesha huduma yao huko New Jersey Marekani. Kama nilivyoandika awali, Freddy ni kijana mwenye kipaji cha hali ya juu, kipaji chake kinaweza kuonekana kwenye album mpya iliyotoka mapema mwaka jana ya kwaya hii maarufu ya The Brooklyn Tabernacle iitwayo "PRAY" ameshiriki katika utunzi wa nyimbo 12 kati ya 14 za album nzima. Kama haitoshi pia ameanzisha ama amesolo nyimbo tano katika album hiyo.

Bishop Freddy na Pam Washington wazazi wa Freddy

KWA TAARIFA YAKO usipomuona Freddy akiimbisha ama akiimba kwenye kwaya basi tazama kwenye benchi la wanamuziki utamkuta akipiga kinanda huko na tabasamu kubwa. Licha ya kuwa na kwaya hiyo kwa zaidi ya miaka mitatu sasa, pia kijana huyu ameshatajwa kwenye tuzo kubwa kama za Grammy, Dove na Stellar zote zinatayarishwa nchini Marekani, ambapo pia licha ya kutoa album yake binafsi lakini pia ameshirikishwa na waimbaji wengine. Watu wengi waliosikiliza album yake walikiri kwamba kijana anauwezo na muziki wake ni waviwango vya hali ya juu.

KWA TAARIFA YAKO Unaweza kumsikiliza kupitia wimbo Jesus unapatikana Youtube ama nyimbo nyingine alizoimba na kwaya yake ya The Brooklyn, ambapo kwaya hiyo ilitarajiwa kutoa DVD yake mwaka jana October kama ilivyosema lakini haijatokea hivyo bado watu wanaendelea kusubiri DVD hiyo ambayo wameweka nyimbo mbili tu Youtube kuwapatia wapenzi wao album itakavyokuwa. Licha ya kuongoza sifa katika kwaya kubwa ya The Brooklyn pia Freddy anaongoza sifa kwa upande wa vijana wa kanisa hilo sambamba na kwaya ya watu wachache ambao husafiri na mchungaji kiongozi wa kanisa hilo endapo wanapata mwaliko iitwayo The Brooklyn Tabernacle Singers, kwakuwa kwaya kubwa haiwezi kusafiri umbali mrefu kwasababu ya ukubwa, watu zaidi ya 250. Kumbuka pia kwaya hii ndio iliyokuwa kwaya rasmi katika kuimba wakati wa kuapishwa kwa Rais Barack Obama muhula wa pili.


The Brooklyn Tabernacle Choir wakati wa "Pray" DVD & CD live recording

Tazama  "At the Cross" uliopo katika DVD mpya ambayo haijatoka ukiongozwa na Freddy

    Freddy akianzisha wimbo "The Great I am" wakati wa ibada ya kawaida kanisani Brooklyn

Freddy akianzisha "Every Praise" utunzi wa Ezekiah Walker, ibadani kanisani Brooklyn TB



SOMO: KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU (3 & 4) - MCHUNGAJI MADUMLA

$
0
0


Kama hukusoma sehemu ya kwanza na ya pili bonyeza hapa

Kama tayari unaweza kuendelea na sehemu ya tatu na ya nne chini. Barikiwa

Karibu tuendelee;

Bwana Yesu asifiwe…

03.AINA ZA KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU.

Karama hizi ni miongoni mwa karama ambazo biblia imeziorodhesha katika 1 Wakorintho 12:8-10. Ili kuelewa vizuri na kupata mpangilio mzuri,basi nimekupangia karama hizi katika makundi makuu manne;

A.Karama za kusema.

(i) Lugha.

(ii) Kutafsiri lugha.

(iii)Unabii.

B.Karama za Ufunuo.

(i) Neno la hekima.

(ii)Neno la maarifa.

(iii)Kupambanua Roho

C.Karama za uwezo.

(i) Karama ya imani.

(ii)Karama za uponyaji.

(iii)Matendo ya miujiza.

Roho mtakatifu ametoa ufunuo mbali mbali kwa kufaidiana kama apendavyo Yeye 1 Wakorintho 12:8.

A.KARAMA ZA KUSEMA.

(i)Karama za lugha

~Karama za lugha nazo zimegawanywa katika sehemu kuu mbili;

Lugha katika kulijenga kanisa, kuhutubu.

Udhihirisho wa Roho wa namna hii ujulikana pia “lugha ya ibada” Hiki ni kipindi cha kuwajenga waamini,kuwatia moyo,kuwatia nguvu kwa maneno yenye kueleweka vizuri (1 Wakorintho 14:3). Sifa mojawapo ya karama hii ni kwamba,ili ifanye kazi inategemea hadhara ya watu walioandaliwa kupokea ujumbe. Kuhutubu,kunamfanya yeye aliye mjinga kupata nafasi ya kuelimika kwa neno la Mungu.

Lugha katika kunena(kunena kwa lugha mpya)

Uhidhihirisho huu ni wa aina ya pili,ni udhihirisho wa Roho mtakatifu katika kunena kwa lugha.Kunena kwa lugha ni kutamka maneno katika Roho yasiyopangwa kutamkika,na yasiyoeleweka maskioni mwa watu hata shetani haelewi kabisaa!isipokuwa roho ya mtu hunena mambo ya siri na Roho wa Mungu~ Matendo 2:4.

Kumbuka;kupo kunena kwa lugha mpya baada ya Roho mtakatifu kushuka (Matendo 19:6,Matendo 2:4) Lakini pia kupo kunena kwa lugha kwa namna ya karama rasmi. Kile ninachozungumzia hapa ni unenaji wa lugha katika karama.

Mtu mwenye karama hii,muda wote aweza kunena kama apendavyo Roho mtakatifu. Haitaji kuanza kutafuta uwepo kwamba aabudu kwa kipindi kirefu ndipo anene,bali anaweza akaabudu kidogo tu kisha akanena,au akawa akinena katika maombi.

(ii) Kutafsiri lugha.

Karama hii inategemea malighafi ya udhihirisho wa Roho mtakatifu wa kunena kwa lugha. Maana ili utafsiri,unahitaji lugha iliyonenwa lakini haikueleweka,au haieleweki katika hadhara husika,ndiposa hitaji la kufasiri hujitokeza. Karama hii inawezeshwa na Roho mwenyewe,kwa sababu hakuna awezaye kufasiri lugha kwa kutumia akili zake mwenyewe pasipo kuongozwa na Roho mtakatifu. Wala hakuna ujanja ujanja unaohitajika katika kufasiri lugha pale lugha mpya itolewayo,ni kwa msaada wa Roho mtakatifu tu.

~Je karama hizi mbili yaani,karama ya kunena katika roho,na kufasiri zinatumikaje?

JIBU;Yapo mazingira mawili ambapo yakupasa kuyajua kwamba ni kipindi gani haswa cha kufasiri lugha na kipindi gani haswa si cha kufasiri lugha pindi mmoja anenapo(na huu ni ufunuo)

Hivyo basi ili tuweze kuyajua haya yote hatuna budi kujua aina za unenaji wa lugha,zipo mbili nazo ni;

(a)Mtu akizungumza na MUNGU wake kwa njia ya lugha.

(b)MUNGU akizungumza na watu wake kwa njia ya lugha.

Tazama,Mtu akizungumza na MUNGU wake kwa njia ya lugha,haitaji mtafsiri maana mtu huyu hunena mambo ya siri katika roho yake,wala hasemi na watu~ 1 Wakorintho 14:2. Lakini,Mungu anaweza kuzungumza na watu wake kwa njia ya lugha akimtumia mtumishi wake,hapa ndipo pana hitaji mwenye karama ya kutafsiri lugha aingie kazini kwa msaada wa Roho mtakatifu ili kuwezesha ujumbe wa Mungu ueleweke kwa watu wote ~ 1 Wakorintho 14:13

(iii)Unabii.

1 Wakorintho 12:10

Hapo zamani mtu mwenye karama hii alikuwa akijulikana kuwa ni “ mwonaji” Imeandikwa“ (Hapo zamani katika Israeli, mtu alipokwenda kuuliza neno kwa Mungu, husema hivi, Haya! Twende kwa mwonaji; maana mtu aitwaye sasa Nabii hapo zamani aliitwa Mwonaji.) “1 samweli 9:

Hivyo basi,karama hii inampa mtu kuona mambo yajayo katika ulimwengu wa roho kwa kadri Roho mtakatifu anavyojifunua kwake. Karama hii ni zawadi nzuri ya kupata taharifa za matukio yajayo,ili uweze kuyashughulikia sasa. Hata kanisa,haliwezi kwenda bila nabii,yeye aonaye mambo ya sirini. Ikumbukwe ya kwamba unabii hautolewi kwa sababu ya mapenzi ya mtu fulani bali kwa sababu ya mapenzi ya Roho mtakatifu;

“ Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.” 2 Petro 1:20-21

(B.)KARAMA ZA UFUNUO.

(i) Neno la hekima.(1 Wakorintho 12:8)

Awali ya yote yakupasa kujua nini haswa maana ya hekima.

Hekima;ni moyo wa adili wa kuhukumu katika haki na ni uwezo wa kupambanua mema na mabaya (1 Wafalme 3:9)

( Ni moyo mwelevu unaotambua kila jambo kwa mtazamo wa kiungu na neno lake. Au hekima ni kunena au kusema jambo sahihi,kwa watu sahihi na wakati sahihi.)

Moyo huu wa adili wa kupambanua mema na mabaya katika haki ndio karama yenyewe ya ufunuo. Lakini hatusemi “ karama ya hekima” bali “ karama ya neno la hekima“. Mfano katika biblia; katika Luka 20:19-26,hapo utaona waandishi na wakuu wa makuhani wakijaribu kumkamata Bwana Yesu kwa hila zao,wakimtega kwa kumuuliza kwamba ni halali wao kumpa kodi Kaisari au la?

tunaona hapo Bwana Yesu akitumia karama ya “neno la hekima ” kuwajibu,na hatimae wale wenye hila walistaajabu na kunyamaa.Mifano mingine katika biblia;Soma Yoh. 8:3-11,Matendo 6:1-5,Matendo 15:25-29,Matendo 27:23-24. N.K

Utendaji kazi wa karama hii ya neno la hekima;

~Uwezesha kufanya maamuzi kwa usahihi na kwa haki.

Mtu mwenye karama hii,anaweza akawaamua na kuwaongoza watu wake kihekima. Kanisa linahitaji karama hii,ili pasiwepo na upendeleo wowote ule.

(ii) Neno la maarifa. 1 Wakorintho 12:8

Neno la maarifa ni mojawapo ya karama ya ufunuo wa Roho mtakatifu wa kujua mambo mbali mbali katika uhalisia wake. Pia, ni sehemu ndogo ya maarifa ya Mungu ndani ya mwenye karama hii. Tuangalie mifano michache kuhusu karama hii ndani ya Bwana Yesu.

Yesu alifahamu kweli iliyopo ndani ya Nathanaeli kabla hata hajakutana naye,imeandikwa;“Basi Yesu akamwona Nathanaeli anakuja kwake, akanena habari zake, Tazama, Mwisraeli kweli kweli, hamna hila ndani yake.Nathanaeli akamwambia, Umepataje kunitambua? Yesu akajibu, akamwambia, Kabla Filipo hajakuita, ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona.” Yoh.1:47-48.

Kupitia andiko hilo,tunaona ya kwamba Yesu akiwa na neno la maarifa kuhusu Nathanaeli wa kana ya Galilaya. Pia waweza kusoma Yoh.4:18-20,(Yesu akiwa na maarifa kamili juu ya mwanamke msamalia kwa kujua yote aliyokuwa nayo kabla ya kukutana naye.),

Soma pia habari za Anania na Safira mkewe, Matendo 5:3,jinsi karama ya neno la maarifa ilivyofanya kazi ndani ya Petro,kiasi cha kujua siri yote aliyoifanya Anania na Safira mkewe katika mauzo ya kiwanja.N.K

Kumbuka;neno la maarifa ni tofauti kabisa na maarifa ya mwanadamu ya asili. Hii ni karama yaani ni utendaji kazi wa Roho mtakatifu katika maarifa yake. Hivyo maarifa haya ni tofauti na maarifa ya kusomea,tena ni tofauti na maarifa ya asili bali ni Roho mwenyewe.

Utendaji kazi wa karama hii;

(a) Kufichua dhambi. ~Matendo 5:1-3

~Kupitia karama ya neno la maarifa,dhambi hufichuliwa. Maovu pia hufichuliwa kwa sababu mwenye karama hii amepewa kuona kimaarifa.

(b) Kuwa na wigo mpana wa kutatua tatizo.

Karama hii,inampa wigo mkubwa muhusika wa kutatua tatizo kwa maana anakuwa na maarifa ya ki-Mungu juu ya tatizo. Kuna kipindi fulani ambacho unahitaji neno la maarifa ili uweze kushughulikia tatizo la kiroho kiundani haswa.

(c) Karama hii inakuwezesha kushauri,kuomba,au kuombea wengine kimapana.

~Tazama, mtu akijawa na karama ya neno la maarifa huweza kujua jinsi impasavyo ya kutoa ushauri mzuri kwa mtu mwenye kuhitaji kushauriwa,kwa maana wakati mshauriwa anaeleza hapo mwenye karama anaweza kujua jambo sahihi la kumshauri na lipi asimshauri kwa maana atakuwa akiona na kuyapima maneno yote ya mshauriwa hata kama hajamaliza kumsimulia. Karama hii ya neno la maarifa itamuwezesha mtumishi ajue namna gani ya kumuombea pia.

(iii)Kupambanua Roho.

~Hii ni mojawapo ya karama ya ufunuo yenye umuhimu sana katika kanisa la leo. Kupamanua roho ni kipawa cha kuzipima roho (is the power of testing spirit)maana nyakati hizi za mwisho zipo roho zidanganyazo(1 Timotheo 4:1). Pia kupambanua roho,ni kipawa cha kuhakiki roho,kuzinyambua nyambua roho. Uwezo huu ni wa umuhimu sana,maana kwa njia ya karama hii ndiposa mtu aweza kutofautisha roho za mashetani na Roho wa Bwana.

Ufanyaji kazi wa karama hii ni kama ifuatavyo;

(a)Kuzipima roho za watu mbali mbali.

Roho za watu mbali mbali zenye kunena habari za Yesu,lazima zipimwe kwa kupitia karama hii. Maana si wote wananena sahihi,bali wengine wengi wamejawa na tamaa zao na wala si watu wa Mungu kwa kazi wazifanyazo. Mfano tuangalie hapa;

“Ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali, kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia bwana zake faida nyingi kwa kuagua. Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akisema, Watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu.Akafanya hayo siku nyingi. Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule pepo, Nakuamuru kwa jina la Yesu Kristo, mtoke huyu. Akamtoka saa ile ile.” Matendo 16:16-18

Kijakazi huyu alikuwa na pepo wa uaguzi,ambapo pepo huyu ni roho ya shetani. Ingawa kile alichokisema kilikuwa sawa maana aliwasemea akina Paulo kwamba ni watumishi wa Mungu aliye hai,wenye kuhubiri njia ya wokovu lakini roho hiyo iliyoyasema ilikuwa ni roho ya pepo,ndio maana Paulo aliweza kumkemea na kumtoa. Paulo aliweza kupamanua roho ndani ya yule kijakazi.

Sasa waweza fikiria kwamba kama Paulo asingelikuwa na karama hii,wewe unafikirije? Je ni kweli angeweza kumkemea? Ukweli ni kwamba angemuacha yule kijakazi aendelee kusema maneno yale,tena angekubali kabisa kwamba waandamane wote katika kuhiubiri injili. Na laiti kama angeambatana naye pasipo kuijua roho itendayo kazi ndani ya yule kijakazi,basi ni dhahiri huduma ya Paulo ingemsumbua baadae.

Na hili ndilo linaloendelea hata leo katika makanisa yetu. Maana wapo watu ni wapunga pepo hali wakijifanya ni watumishi wa kweli. Na kwa sababu ya kuikosa karama hii,tumejikuta tukiwakumbatia watu hao na kuwapa nafasi mbali mbali za kiutumishi~ sasa mwishoe hatujui ipi miujiza ya kweli,na ipi ni ya uongo kwa sababu ya kushindwa kupambanua roho.

(b)Kuzipima roho za watumishi wa Mungu.

~Wapo watumishi wa Mungu wa ukweli ambao hufanya kazi ya Mungu kihusahihi kabisa. Lakini baadhi yao wanaweza wakatumiwa na roho za kishetani pasipo wao kujijua ya kwamba wanatumika kipindi hicho,inawezekana katika kipindi hicho cha kutumika na roho mbaya wao wakawa wamejisahau,labda waliruhusu hasira,uchungu,magomvi,hofu.N.K,

hivyo hayo yote yakawa ni mlango wa shetani,kisha roho ya pepo ikaingia ndani yao. Hapo sasa roho itakayotenda kazi kipindi hicho siyo Roho mtakatifu bali ni roho mtakafujo roho ya shetani hali mtumishi huyo ni wa Mungu. Tumeona mara nyingi maneno mabaya yakiwatoka watumishi wa Mungu,mpaka tunashangaa kwamba ni kweli mchungaji huyu huyu tunayemfahamu?!! Au mwingine,?!!

Mfano tuangalie hapa;

“ Tangu wakati huo Yesu alianza kuwaonya wanafunzi wake ya kwamba imempasa kwenda Yerusalemu, na kupata mateso mengi kwa wazee na wakuu wa makuhani, na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu kufufuka.Petro akamchukua, akaanza kumkemea, akisema, Hasha, Bwana, hayo hayatakupata.Akageuka, akamwambia Petro, Nenda nyuma yangu, Shetani; u kikwazo kwangu; maana huyawazi yaliyo ya Mungu, bali ya wanadamu.” Mathayo 16:21-23

Petro alikuwa si shetani,bali ni mtumishi wa Mungu kweli kweli. Lakini katika andiko hili tunaona Yesu akamwambia “Nenda nyuma yangu,shetani;u kikwazo kwangu...” Yesu aliweza kutambua ya kwamba roho iliyokuwa ikitenda kazi saa ile haikuwa roho ya Petro bali ilikuwa ni roho ya shetani.

Si Roho yule wa Bwana kwa kipindi kile bali ni roho ya shetani ndio ilikuwa ikinena ndani ya Petro,Yesu akaipambanua kisha akatambua. Ikumbukwe kwamba Yesu alipoanza kuwaonya juu ya mateso yake,huyu Petro aliingiwa na hofu,kumbuka ;hofu ni mlango wa shetani,hivyo Petro aliweza kufungua mlango na roho mbaya ikamuingia ndiposa akaanza kumkemea Yesu kwa kuyakataa yale ambayo Yesu alikuwa akiwaambia.

Katika eneo hilo,si rahisi kujua roho ya shetani na Roho wa Mungu ikiwa kama huna karama hii ya kupambanua roho. Karama hii ikikosekana,wengi hunaswa katika roho za miujiza ya shetani wakidhani ni ya Mungu….

ITAENDELEA…
~ Kwa huduma ya maombezi,tafadhali usisite kunipigia simu yangu hii;+255 655 11 11 49.

Mchungaji Gasper Madumla.

Beroya bible fellowship church(Kimara,Dar,TZ)

UBARIKIWE.

SITTA ALIBARIKI TAMASHA LA PASAKA

$
0
0
Na Mwandishi wetu,
Samuel Sitta
Aliyekuwa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, ametoa wito kwa waandaaji wa Tamasha la Pasaka, Kampuni ya Msama Promotions kutosahau kwaya za makanisa mbalimbali.

Kwa mujibu wa Sitta, Msama wanatakiwa wasiweke mkazo kwa waimbaji binafsi pekee bali pia na kwaya za makanisa ambazo mchango wake nao unatambulika.

Sitta pia anampongeza Alex Msama baada ya tamasha hilo kwa namna mapato yake yanavyosaidia makundi yenye uhitaji maalum kama yatima, wajane na walemavu ambao mara nyingi husahaulika.


Sitta amesema matamasha hayo yana malengo mazuri kwa watanzania, hivyo wadau wanatakiwa kumuongezea nguvu katika ufanikishaji wake.

Kwaya za Katoliki, Lutherani, Assemblies of God na nyinginezo sambamba na Kwaya za nje ni muhimu kuwepo ili kubadilishana uzoefu kati ya kwaya za Tanzania na nje.

"Miaka ya hivi karibuni, Kwaya za makanisani tumezisahau, tuzitumie kwa sababu nazo ni eneo letu," anasema Sitta.

Naye Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ameeleza kuhusu kupokea mawazo ya Sitta ambayo ni ya muhimu, hivyo Kamati ya maandalizi wanayafanyia kazi maombi ya wadau mbalimbali ili kuliboresha zaidi.

Msama alisema hivi sasa wanasubiri kupatikana kwa kibali kutoka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ili kuendelea na taratibu za kufanyika kwa tamasha hilo.

SOMO: JE WEWE NI WEWE? - MCHUNGAJI MACHUMU

$
0
0

Mchungaji Maximilian Machumu (Kanisa Ufufuo na Uzima)
Somo : Je wewe ni wewe? 

Malaki 3:1 Imeandikwa:- 1 "Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi."


Malaki 4: 5 "Angalieni, nitawapelekea Eliya nabii, kabla haijaja siku ile ya Bwana, iliyo kuu na kuogofya. Naye ataigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto wao, na mioyo ya watoto iwaelekee baba zao, ili nisije nikaipiga dunia kwa laana."
Malaki anaelezea juu ya mjumbe wa pili Eliya. Unaweza kujiuliza Eliya alishaletwa na akafanya kazi yake na kupaa kwenda mbunguni."

Luka1: 11 "Akatokewa na malaika wa Bwana, amesimama upande wa kuume wa madhabahu ya kufukizia. Zakaria alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia. Lakini yule malaika akamwambia, Usiogope, Zakaria, maana dua yako imesikiwa, na mkeo Elisabeti atakuzalia mtoto mwanamume, na jina lake utamwita Yohana. Nawe utakuwa na furaha na shangwe, na watu wengi watakufurahia kuzaliwa kwake. Kwa sababu atakuwa mkuu mbele za Bwana; hatakunywa divai wala kileo; naye atajazwa Roho Mtakatifu hata tangu tumboni mwa mamaye. Na wengi katika Waisraeli atawarejeza kwa Bwana Mungu wao. Naye atatangulia mbele zake katika roho ya Eliya, na nguvu zake, ili kuigeuza mioyo ya baba iwaelekee watoto, na kuwatilia waasi akili za wenye haki, na kumwekea Bwana tayari watu waliotengenezwa."

Zakaria ameambiwa atamzaa mtoto na jina lake atamwita Yohana ambaye atakuwa na nguvu zile zile za Eliya na kazi yake itakuwa ni kugeuza mioyo ya watu imrudie Baba.
Hapa tunaona mtu mwingine aliye ndani ya mtu. Duniani kulikuwa na kazi ya kugeuza mioyo ya watu, watu walimtambua kwa kumwangalia tu mwilini kama Yohana lakini mbinguni walimtambua kama Eliya.

Mtu huyu alikwenda jangwani akawa anakula asali na nzige, vilevile kama Eliya alivyokuwa anaishi jangwani. Mtu huyu alikuwa ni mtu mzuri japo alikuwa anaishi ndani ya mwili wa mtu mwingine. Hii na kwamba hata mtu mbaya pia anaweza akaishi ndani ya mwili wa mtu na kufanya mambo mabaya.

Mathayo 17: 9 "Na walipokuwa wakishuka mlimani, Yesu aliwaagiza, akasema, Msimwambie mtu ye yote habari ya maono hayo, hata Mwana wa Adamu atakapofufuka katika wafu. Wanafunzi wake wakamwuliza, wakisema, Basi kwa nini waandishi hunena ya kwamba imempasa Eliya kuja kwanza? Naye akajibu, akawaambia, Kweli Eliya yuaja kwanza, naye atatengeneza yote, ila nawaambia, ya kwamba Eliya amekwisha kuja, wasimtambue, lakini wakamtenda yote waliyotaka. Vivyo hivyo Mwana wa Adamu naye yuaenda kuteswa kwao."

Wanafunzi wa Yesu walikuwa wameshasoma maandiko na wakatambua kuwa kabla yeye hajaja ilibidi aje Eliya kwanza halafu yeye ndio aje lakini Bwana Yesu aliwajibu vizuri kuwa Eliya alishakuja lakini wao hawakumtambua.
Kwa ufahamu huu kwenye maisha yetu ya kawaida mchawi anaweza kuja kwenye familia bila kumtambua. Unaweza kumwona mtu anafanya mambo ya ajabu anaongea maneno machafu na anatabia mbaya kumbe ndani yake sio yeye kuna mtu mwingine ndiye anayeyafanya hayo yote.

Tumeona Eliya alikuja akawa anafanya mambo makubwa kwa ujasiri kama alivyokuwa anafanya kwenye agano la kale. Tumeona alikuwa anafanya kazi yake ya kuigeuza mioyo ya watu imwendee Baba na baadaye akauwawa.

Mathayo 1: 23 Imeandikwa: "Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi."

Mathayo 2: 1 Imeandikwa: "Yesu alipozaliwa katika Bethlehemu ya Uyahudi zamani za mfalme Herode, tazama, mamajusi wa mashariki walifika Yerusalemu, wakisema, Yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? Kwa maana tuliiona nyota yake mashariki, nasi tumekuja kumsujudia."

Tumeona amezaliwa mtu asilimia mia moja na Mungu asilimia mia moja, alikuwa anakula kama wanadamu na anatenda kama Mungu. Waliofahamu Yesu mtu ambaye ndani yake ni Mungu walikuwa ni mamajusi. Kibinadamu walifahamu huyu mtoto ni mtu lakini ndani kuna Roho ambayo ndiyo ya muhimu sana kuliko mwili wake ndio maana mamajusi walienda kumsujudia kama Mfalme.

Kwenye maisha yetu ya kawaida kuna watu ambao ndani yao kuna roho ambazo ni za kuzimu zimeingia ndani ya familia za watu na kuharibu maisha yao. Elimu hii ndiyo tunayoishughulikia sababu watu wengi wanaishi lakini ndani yao kuna roho ambazo zinawatesa na kupindisha kusudi la maisha yao lisitimie.

Tumeona Bwana Yesu alizaliwa duniani kwenye holi la Ng'ombe na akaishi na watu mpaka alipofika miaka 30 ndipo alipoanza kufanya kazi yake iliyomleta hapa duniani lakini watu alioishi nao hawakumtambua japo mamajusi ambao walikuwa ni wachawi walimtambua yeye ni nani na kumwelezea kama mfalme.
Hii inatufundisha kwamba wachawi wanatambua sana kwamba mtu anaweza akawa anaishi kumbe sio yeye, wanaweza kumchomoa mtu ndani na wakaingia ndani yake au kuweka roho ya kuzimu ndani yake na mtu huyo akawa anafanya mambo mabaya ya ajabu.

Mfano: kwenye ndoa unaweza ukawa unaishi na mke/mume akawa anafanya vitu ambavyo sio vya kindoa na wewe ukaamua kwenda kwa washauri nao wakakuambia unatakiwa uishi naye kwa akili, ukaamua kuishi naye kwa akili laki ni mambo yakawa bado magumu mkeo/mmeo haeleweki. Kwenye ulimwengu wa rohoni unatakiwa utambue kwanza mtu huyo ni yeye au sio yeye ili umshungulikie mkeo/mumeo ambaye anafanya mambo ya ajabu uondoe roho zote zilizoingia ndani yake na mtu aliyeingia ndani yake ili akukomeshe na umpate yeye wa asili.

Mungu anaishi kwenye ulimwengu wa Rohoni ambao ni halisi na sisi tunatakiwa tutambue sisi ni Roho ambazo zinakaa ndani ya nyumba ambazo zinaitwa mwili. kwenye hii dunia shetani ameamua kuhamia ndani ya mwili wa mwanadamu ili atende kazi zake sababu watu wengi wanayafukuza mapepo kwenye miili ya wanadamu, na kusahau kwamba sio mapepo tu yanayoweza kukaa ndani ya miili ya watu,bali hata wachawi pia wanaweza kukaa ndani ya wanadamu.

Kwenye mambo ya Rohoni, zipo ngazi za nguvu, na Roho wa Mungu nguvu ni namba moja, roho ya mwanadamu ni namba mbili na wa tatu ni Makerubi na maserafi. Ngazi ya mwisho kwa nguvu ni malaika akiwemo shetani na malaika zake.

Mungu akitaka kazi fulani ifanyike anatumia Binadamu na malaika, vilevile shetani naye akitaka kufanya kazi anatumia mapepo na wanadamu. shetani sasa hivi ametambua kwamba mapepo anayoyatuma kuharibu wanadamu yanapigwa kwa damu ya Yesu sasa hivi ameamua kutumia wanadamu wa kawaida ambao wanatembea.

Watu wengi hawafahamu Elimu hii na maombi yao yanakuwa ya kawaida sana wakidhani Mungu atatenda bila wao kupigana rohoni.

Dalili ya mtu ambaye sio wa kawaida.

1. Kusikia sauti isiyo ya kawaida ambayo inakuelekeza kufanya mambo fulani. sauti hiyo inakuwa inakuongoza kutenda matendo ambayo hata wewe mwenyewe hupendi kuyafanya lakini unajishangaa kwanini unayafanya. maana yake kuna mtu ndani ambaye anakulazimisha ufanye kama vile anavyotaka yeye. akili yako inakuambia jambo hili ni baya sio zuri lakini unashindwa kujizuia.

2. Mawazo ya kujiua au kufanya hatari mbalimbali. kama ulishawahi kuona mtu anataka kujiua fahamu kuwa kuna mtu ndani yake ambaye anataka kumuua ili aupoteze mwili wake na yeye aliyechukuliwa asirudi ndani ya mwili wake. unaweza kuona mtu anafuata hatari bila kuogopa kumbe mtu huyo anaongozwa na mtu mwingine aishiye ndani yake ili auwe mwili wake.

Watu wanaofanya mambo haya ya kuingia ndani ya watu wanamahesabu yao jinsi ya kuwateka watu wenye nyota nzuri. watu hawa huwa wanaanza urafiki na wazazi au ndugu ili waweze kuingia ndani ya watu ambao nyota zao zinang'aa sana, watumie akili zao, wafanye mambo ya kishetani bila watu kufahamu na kudhani ya kuwa ni mtu amebadilika kumbe ni wale waishio ndani wanosababisha. Ashukuriwe Mungu muumba mbingu na nchi ambaye ametufunulia Elimu hii na kutupa uwezo wa kutoka kwenye vifungo hivi kwa jina la Yesu.

3. Magonjwa yasiyoeleweka/ ya ajabu ajabu/ yasiyotibika. Unaweza kujiuliza kwanini mtoto amekua tumboni ametoka nje ya uzazi na wanasayansi wanakuwa na maelezo yao kumbe ni mtu ambaye ameingia kwenye ulimwengu wa rohoni na kufanya hayo yote.

Unaweza kukutana na mtu kwenye mahusiano ambaye ukimwelezea mambo ya kuoana anakuwa hakuelewi lakini kwenye mambo ya beach, kutoka out, anakuelewa vizuri sana, ukimweleza kuhusu mambo ya mahubiri, au Biblia inasemaje mtu huyo anakuwa hakuelewi na mara nyingi kwenye maombi anakuwa haombi hata kama unakwenda naye kanisani anakuwa haombi yeye anasubiria kusema amen. Mtu kama huyu ni mtu ambaye hana malengo na wewe bali anakutafuta ili aharibu maisha yako.

Watu wengi wameingia kwenye mahusiano na watu ambao wameharibu maisha yao bila wao kufahamu kumbe ni mfumo wa kishetani ambao umejengeka duniani ili kuharibu maisha yao na kusudi lao.

Namna ya kumkomesha mtu akiwa ndani ya mtu.

Usiamini kila Roho bali kila roho mzijaribu. Fanya maombi ukijua mtu ndani ya mtu ndiye anayekusumbua. Unatakiwa ufikie mahali usiamini kila roho unayokutana nayo bila kufanya maombi. Kama mtu hayumo ndani yake unamwita njoo na anakuja.

Uchawi umefika mahali ambapo unapambana na akili za kibinadamu unapambana na mazingira, hospitali, maombi unajua kabisa mtu anaweza kwenda kuomba. kinachowachanganya wachawi ni kutokujua maombi yanayokwenda kufanyika pale mtu anapokwenda kanisani.

CHAGUO LA GK: NINA HAJA NAWE YA DIAT NA LILY EDWARD

$
0
0
Tunatumai u mzima mdau wa Gospel Kitaa kwa Jumapili ya leo tarehe 24 Januari 2016. Kati ya yote tunayofanya tunatambua ya kwamba hakika tuna haja na Yesu mwokozi wetu aendelee kutufanya tudumu katika uwepo wake na kupata baraka zote za duniani.

Chaguo la GK leo tuko na kinadada ndugu, Diat na Lily Edward, katika video iliyoongozwa na mmojawapo wa wana Team GK, John Maulid. Kinadada hawa wanatukumbusha namna gani hatuwezi kwenda kivyetu vyetu bila msaada wa Mungu.


Tunakutakia Jumapili njema
Viewing all 1245 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>