Quantcast
Channel: Gospel Kitaa™
Viewing all 1245 articles
Browse latest View live

SHANGWE ZA GK: SHUKRANI BAADA YA TAMASHA LA FURAHA ISAYA

$
0
0
Boxing Day ama siku ya kufungua zawadi ilikuwa ni siku ambayo Furaha Isaya alizundua single yake. Baada ya tukio hilo la uzinduzi, Furaha ambaye pia ni mwana One Voice Family International, aliweka kambi pamoja na wanakikundi wenzake nyumbani kwa Lilian Kimola, ambao ilikuwa ni shangwe kwa kwenda mbele pamoja na kumshukuru Mungu.

Zifuatazo ni picha za tukio

Vicktory Syaona Na Magreth Mwakyusa

Mkolosai Na Vick Wa PPR

Magreth Na Furaha Isaya

OVF

John Wa JM Media Na Joyce Ombeni

Joyce Ombeni

Magreth Mwakyusa


Elie Na Vicky


Furaha Isaya

Furaha na Joyce Ombeni

Noel Migongo Na Furaha Isaya


Furaha Akimlisha Keki Mtoto

Furaha Akimlisha Keki Magreth

Furaha Akimlisha Keki Kenny Mavoko

Pastor Beny toka Arusha Akilishwa keki Na Furaha Isaya

Furaha Isaya Akimlisha Keki Bony Kazi Wa Team Gk

Nyorobi Akilishwa Keki Na Furaha Isaya

Nyorobi Akimlisha Keki Vicky Wa PPR

OVF wakila Mishikaki Pamoja na Keki

Liliani Kimola Akilishwa Keki na Furaha Isaya

Elie wa Team GK Akimlisha Keki Furaha Isaya

Elie Wa Team GK Akijiandaa kumlisha Keki Furaha

Mch. Mkolosai

Magreth Na Elie Wa Team GK

Bony Kazi Wa Team GK

Mch. Joshua Silomba, Lilian Kimola, Furaha Isaya Na Noel Migongo

Lilian Kimola, Furaha Isaya na Noel Migongo

Pastor Beny

OVF wakipata chakula

Vicky Wa PPR

Mkolosai

John Maulid Wa Team GK

OVF

Furaha Isaya Na Noel Migongo

Kenny Mavoko

Preshaz

Mch. Joshua Silomba

Noel Migongo

Pastor Benny

OVF



CHAGUO LA GK TUANZE MWAKA KWA SHANGWE ZA KUMSIFU MUNGU WETU

$
0
0


Katika kuanza mwaka kwa kishindo tunaanza na wimbo wa kusifu mpya kabisa kutoka kundi mahiri katika medani ya muziki wa injili nchini Tanzania, wakifahamika kama Glorious Worship Team kupitia wimbo wao 'Bwana wa Majeshi'. Tumekuchagulia wimbo huu ikiwa kama chaguo letu kwako katika kumshukuru Mungu kutuvusha salama kutoka mwaka 2015 - 2016. Hakika ni kwa neema na rehema tu kwa nafasi hii. Basi tukutakie jumapili njema unapoutazama wimbo huu na kusikiliza maneno na muziki wake namna ulivyopangiliwa vyema.


SOMO: UMUHIMU WA NENO LA MUNGU - MCHUNGAJI MADUMLA

$
0
0


Na mchungaji Gasper Madumla.

Bwana Yesu asifiwe…

Zipo faida nyingi sana za neno la Mungu maishani mwetu,faida hizi ni nyingi mno kiasi cha kushindwa kuzieleza zote hapa. Lakini tuangalie faida kumi na tano (15) tu ambazo nazo ni chache kati ya nyingi zilizopo.

~Awali ya yote ikumbukwe kwamba neno la Mungu katika biblia ni sauti ya BWANA MUNGU iliyohifadhiwa kwenye maandishi. Ni MUNGU mwenyewe akizungumza na wote wenye mwili.

Sauti hii ya Mungu imekusudiwa kwetu katika Kutufundisha,kutuonya makosa yetu,kutuongoza katika njia sahihi na kutuadabisha katika haki~ 2 Timotheo 3:16

Tunapaswa kujifunza na kulitii neno la Mungu kila siku iitwapo leo kwa maana katika neno la MUNGU ndipo tunazungumza na MUNGU na ndipo mahali ambapo tunakamilishwa ukristo wetu. Tuangalie umuhimu wa neno la MUNGU kama ifuatavyo;

01. NENO LA MUNGU LINA UZIMA.

~Neno la MUNGU ni la uzima,lenyewe ni roho kamili iletayo uzima wa kiroho ~Yoh.6:63.

Pia kumbuka ya kwamba Yesu ni neno,anasema Yeye ndio njia kweli na uzima.(Yoh.14:6). Kwa lugha nyepesi ni kwamba mtu akiwa ameketi katika neno la Mungu la usahihi,mtu huyo amepewa uzima maana atakuwa ameketi ndani ya Yesu yaani ndani ya neno.

02. LINATOA NAFASI YA UTENDAJI KAZI WA ROHO MTAKATIFU.

~Hii ni siri kubwa ya utendaji kazi wa Roho mtakatifu. Roho mtakatifu hutenda kazi katika neno lake. Ukisoma hapo katika kitabu cha Mwanzo 1:1-3,utagundua kwamba neno lilipotamkwa ndipo Roho mtakatifu naye akaingia kazini kulitimiliza. Hata leo ni vivyo hivyo.

03.LINAUMBA.

~Tunajua ya kwamba ulimwengu uliumbwa kwa neno la Mungu.(Waebrania 11:3). Hapo utagundua pia neno la Mungu litokalo kinywani mwako linafanya kazi ile ile ya kuumba ndio maana tukitamka neno la uponyaji,uponyaji ufanyika,tena tukitamka neno la kuvuka,tunavuka kwa jina la Yesu Kristo.Soma pia ~( Zab.33:6,9 )

04.LINAPONYA.

Bwana Yesu alitamka neno kwa wadhaifu,nao wakapona. Sisi nasi leo,twataamka neno la Mungu kwa wadhaifu,wagonjwa nao hupona. Ukisoma katika Mathayo 8:7-8,13. Pia Matendo 14:8-10. Maandiko hayo yote mawili yanaonesha kwamba neno la Mungu linaponya,ona~Yesu alitamka kisha mgojwa akaponywa pia Paulo naye alitamka neno kwa yule kiwete naye akaenda saa ile ile.

05.LIMEBEBA MIUJIZA YA KWELI.

~Suala la miujiza lipo hata kwa shetani lakini ukweli ni kwamba miujiza ya Mungu ndio miujiza ya pekee yenye ukweli kwa sababu imejengwa katika misingi ya neno la Mungu,(tazama hili katika miujiza ya Musa na ya wale waganga, maana Musa alifanya nyoka,nao wakafanya nyoka lakini nyoka wa Musa akawala nyoka wao.shetani anaweza akafanya ajabu fulani,lakini muujiza wa Mungu ni mkuu kuliko hiyo ya shetani.)Tazama neno la Mungu lilivyobeba miujiza na ishara~Marko 16:20

06.LINATAKASA ROHO ZETU.

Imeandikwa“Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.”Yoh.15:3. Andiko hilo linatuonesha ya kwamba usafi uliofanyika hapo umetokana na neno la Mungu.

Lakini pia imeandikwa “ Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake; ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;” Waefeso 5:25-26

07.LIMEBEBA UWEZA NA NGUVU.

Ipo tofauti kati neno uwezo,na neno uweza. Uwezo ni nguvu fulani ya kawaida ya utendaji kazi,lakini uweza ni nguvu ya ki~ungu,ambayo hakuna mwenye nayo isipokuwa MUNGU tu. Uweza huu upo pia katika neno lake MUNGU. Neno la Mungu linapotamkwa basi ujue ipo nguvu ya utofauti kabisa ifanyayo kazi na lile neno.( Mwanzo~Ufunuo)

08.NENO LA MUNGU NI KWELI YOTE.

Kama vile tulivyoona hapo juu ya kwamba neno la Mungu linatakasa,maana neno lake ndio kweli ~Yoh.17:17. Hakuna mahali pengine ambapo tutapata kweli yote isipokuwa ndani ya neno la Mungu tu.

09.HUTUTUNZA KWA USAFI.

~Wale waliookoka,kisha wakadumu katika neno la Mungu hujikuta wakizichukia dhambi walizokuwa wakizifanya hapo awali. Na kile kinachowafanya kuchukia dhambi ni kiwango cha neno la Mungu ndani yao. Zab.119:11

10. LINAHUSIKA KUTUZAA UPYA KWA MARA YA PILI.

~Mpendwa,nje ya neno la Mungu hakika hakuna awezaye kuokoka. Maana inawezekanaje mwenye dhambi akaokoka pasipo kuvutwa na lile neno la Mungu? Basi sharti alisikie neno ndipo afanye maamuzi. “Kwa kuwa mmezaliwa mara ya pili; si kwa mbegu iharibikayo, bali kwa ile isiyoharibika; kwa neno la Mungu lenye uzima, lidumulo hata milele.” 1 Petro 1:23

11.NENO LA MUNGU LINAKUZA ROHO ZETU.

~roho zetu hazikui kwa chakula cha kibinadamu bali zinakuwa kwa chakula cha kiroho ambacho ni neno la Mungu. Hivyo kama tujuavyo kazi ya chakula ni kumkuza mtu,kumpa nguvu,kumpa kuishi. 1 Petro 2:2

12.NENO LA MUNGU NI SILAHA DHIDI YA NGUVU ZA GIZA.

~Yesu alimshinda shetani kwa neno tu ( Mathayo 4:1-11) Ikiwa Yeye Bwana alimshinda shetani kwa neno la Mungu basi nasi ni lazima tutumie silaha hii ya neno la Mungu; ili tumshende shetani,Soma tena Waefeso 6:17 N.K

13.NENO LA MUNGU NI MBEGU IPANDWAYO MIOYONI MWETU.

~“Na huo mfano, maana yake ni hii; Mbegu ni neno la Mungu.”Luka 8:11 Soma habari ya mpanzi yote~Mathayo 13:1-43

Tarajio kubwa kwa mbegu iliyopandwa ni kukua na kuongezeka.

14. LINATUPA NGUVU YA KUOMBA.

~Ikumbukwe kwamba neno ni mbegu,maombi ni kama maji. Mbegu pasipo maji kamwe haikui,bali hufa pia maombi pasipo neno la Mungu hayana muelekeo mzuri. Neno la Mungu litakuongoza katika maombi yako ya kwamba nini cha kuomba na nini si cha kuomba kwa wakati. Tazama maisha ya akina Danieli,Hanania,Mishaeli na Azaria,wakaomba ,maana walikuwa na maarifa ( Danieli 2:17-19)

15. NI CHAKULA CHA ROHO ZETU.

~ Mwili hulishwa kwa chakula cha kibinadamu,roho hulishwa kwa neno. Mtu hataishi kwa mkate tu ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu~ Mathayo 4:4

~Hayo ni machache kati ya mengi,nimeona nikuandikie hayo ili uyapate kuyajua. Lakini wapo watu ambao wana ugumu mkubwa sana wa kusoma neno la Mungu. Wengine wakianza kusoma tu,mara husinzia. Wengine wakisoma hawaelewi hata kidogo,uchovu gafla uwakamata. Naomba ukiwa wewe ni mmoja wapo kati ya watu wa namna hiyo,naomba unipigie simu hii;+255 655 11 11 49.

Mchungaji Gasper Madumla.

Beroya bible fellowship church(Kimara,Dar,TZ)

UBARIKIWE.

MIKOA YAGOMBANIA TAMASHA LA PASAKA 2016

$
0
0
Sipho Makhabane "The Big Fish" kwenye tamasha la pasaka 2013 jijini Dar
Na Mwandishi Wetu

Wananchi wa mikoa mbalimbali wamejitokeza kuiomba kkampuni ya Msama Promotions ianzie Tamasha la Pasaka mikoa kwao mwaka huu huku wakazi wa dare s salaam wakisisitiza libaki mkoani humo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Alex Msama ameliambia Gazeti hili kuwa, tayari amepokea maombi toka kwa wananchi na mashabiki wa mikoa ya Morogoro, Mwanza, Mbeya, Dodoma na Dar es Salaam wakitaka tamasha hilo lianzie kwao mwaka huu.

“Kamati yangu inafuata taratibu za Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) ambazo ni pamoja na kupata kibali cha kufanikisha kufanyika kwa Tamasha hilo linaloshirikisha waimbaji mbalimbali wa muziki wa Injili wa ndani na nje ya Tanzania,” amesema Msama.

Salum Ismail Hamad ambaye ni mdau mkubwa wa Tamasha la Pasaka amesema anawaomba waandaaaji wa Tamasha hilo kutoliondoa jijini Dar es Salaam kwa sababu ni mkoa unaohusisha idadi kubwa ya mashabiki wa muziki wa Injili.

Rukia Joseph wa Kimara Dar es Salaam, alisema yeye anawapigia magoti waandaaji kutoliondoa tamasha hilo jijini Dar es Salaam hasaa kwa waimbaji wa nje ya Tanzania kama Solly Mahlangu na wengineo toka nje ya nchi.

Michael Deogratius alisema ni ngependa Tamasha la Pasaka lihamie mikoani kwa sababu ya ukubwa na umuhimu wa tamasha hilo ambalo linatimiza miaka 16 tangu kuasisiwa kwake.

Msama alisema bado wanasubiri taratibu za kufanikisha tamasha hilo kutoka Basata, hivyo nawaomba wakazi wa mikoani kuvuta subira wakati wakijiandaa.

2016 NI MWAKA WENYE TIJA

$
0
0
Na Askofu Sylvester Gamanywa
WAPO Mission International.



Leo natabiri kwamba mwaka 2016 ni mwaka wenye tija! Utaniuliza nimejuaje? Kama wewe huamini subiri uone kwa macho ila tu kwako binafsi, kwa kutokuamini kwako, hautakuwa na tija kwa sababu utakuwa umepoteza muda wako ukisibiri kuona ni jinsi gani huu ni mwaka wenye tija. Tafsiri ya Kiswahili sanifu kuhunu neno “tija” maana yake ni “matokeo mazuri yenye faida.”! Unajua kwamba kuna mambo mengi yanayofanyika, tena yanatumia gharama kubwa, lakini hayaleti “matokeo mazuri yenye faida.”

Muda ni kwa ajili ya binadamu na
sio binadamu kwa ajili ya muda

Kumbuka tunaposema habari za mwaka tuna maana ya “kipindi cha miezi kumi na mbili, kuanzia Januari mpaka Desemba.” Hiki ni kipindi cha matumizi ya muda. Kwa asili muda ni “amana” yaani kitu cha thamani kubwa. Muda ukipangwa na kutumiwa vizuri, kuanzia Januari mpaka kuja kufika Desemba lazima utaleta “matokeo mazuri yenye faida.”

Kwa mantiki hii, muda umetolewa kwa ajili ya kumwezesha binadamu kutimiza kusudi la Mungu la kumleta duniani. Binadamu hakuumbwa kwa ajili ya kutumikia muda. Muda umewekwa kwa ajili ya binadamu kulitumikia kusudi la Mungu.

Sasa hebu nikushirikishe ni kwa jinsi gani mwaka 2016 utakuwa ni mwaka wenye tija. Naomba turejee kwenye kitabu cha kwanza katika Biblia, sura ya kwanza ili tuone chimbuko la kile kinachoitwa “Baraza za Mwenyezi Mungu” kwa binadamu wa kwanza kama ilivyoandikwa:

Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha; mkatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na kila kiumbe chenye uhai kiendacho juu ya nchi….” (MW.1:28)

Katika maandiko haya naomba tuchukue haya maneno 3 ambayo ni 1. Zaeni, 2. Mkaongezeke, 3. Mkaijaze nchi na kuitiisha. Kila neno hapa liana uzito wake maalum na ni muhimu tuuzingatie ili kuweza kujua kuna ujumbe gani.

1.    Zaeni- kanuni ya ubunifu na uzalishaji

Wengi wana tafsiri ya binadamu kuzaana wenyewe kwa wenyewe. Hii ni tafsiri finyu sana. Kimsingi neno zaeni linawakilisha kanuni ya “ubunifu na uzalishaji”! Mungu alipowatamkia mbaraka binadamu wa kwanza, aliwatabiria kuhakikisha kazi ya uumbaji wa viumbe na uzalishaji wa mimea na mifugo vinaendelea kufanyika pasipo kuhusisha mkono wa Mungu moja kwa moja.

2.    Mkaongezeke – kanuni ya kuongezeka

Haya kanuni ya ubinufu na uzalishaji unahusika kwenye kupata wazo jipya la kufanya kitu kipya na kulifanyia kazi ili kuleta hicho kitu kipya kwenye ulimwmengu wa asili. Lakini kanuni ya kuongezeka inahusika zaidi na kile kinachotumika katika kuzalisha kisizalishe vichache bali kitumie kanuni ya kuzidisha kwenye uzalishaji. Maana yake ukipanda mbegu moja ardhini, itakapoota na kuzaa zipatikane mbegu kama ile iliyopandwa zikiwa nyingi hata mara mia moja. Kama ulifunga mbuzi au ng’ombe au kuku wakati wanapozaa, wazae zaidi ya mmoja na katika muda mfupi, idadi yao iongozeke kwa kanuni ya kuzidisha na sio kujumlisha.



3.    Kujaza nchi na kuitawala – Kanuni ya kumiliki

Kujaza nchi na kuitiisha na kutawala yote yanawakilisha mamlaka ya kumiliki ardhi na mali. Kumiliki ndiko kunakotimiza kusudi la Mungu kumuumba binadamu la “kutawala”! Kumbuka kwamba kanuni ya kutawala inalenga kutawala viumbe hai, ardhi na mazingira yake, lakini sio “kumtawala binadamu”! Pili, kila binadamu alikuwa na fursa hii ya kuzalisha na kuzidisha na “kumiliki uchumi” kama sehemu ya Mbaraka wa Mungu kwa binadamu. Suala la binadamu kumtawala binadamu mwenzake ni matokeo ya anguko la bunadamu katika dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.

Kupitia uchambuzi uliotangulia hapa juu, tunapata picha kwamba, Baraka za Mungu kwa binadamu hazikutarajiwa kumfikia akiwa amelala bustanini bali alitakiwa kufanya kazi maalum. Ubunifu wa kupata wazo jipya na kulitendea kazi liwe kitu halisi hii ni kazi. Kusimamia mchakato wa uzalishaji unaoongezeka nayo ni kazi. Hata kukusanya na kusimamia milki nayo pia ni kazi. Hakuna mahali mtu atakaa abweteke halafu mambo yanajiendesha yenyewe pasipo ushiriki wake.

Imani na uchumi
havitenganishwi

Lakini jambo jingine la kujikumbusha hapa ni kwamba, Kusudi la Mungu kumwumba binadamu ni kutawala nchi kwa kwa niaba ya Mungu. Na utawala uliotajwa ni wa viumbe, ardhi na mazingira yake. Maana yake “kutawala matunda ya uchumi” unaotokana na rasrimali asilia za Mungu mwenyewe. Na hii ndiyo inatuleka kwenye kipengele kingine muhimu kinachogusa “Imani na uchumi havitenganishwi”!

Sijui ni nani mwasisi wa kitheolojia aliyeanzisha nadharia ya kutenganisha “imani na uchumi” katika dini ya Kikristo. Utafiti wangu katika Biblia kuanzia kitabu cha Mwanzo mpaka ufunuo, sina kifungu wala andiko linalotenganisha “imani na uchumi”! Labda nifafanue ni nini ninacho maanisha kuhusu “imani na uchumi”.

Imani ni uhusiano binafsi kati ya binadamu na Mungu. Ni mfumo wa maisha yanayotegemea uongozi na Baraka za zitokazo kwa Mungu. Pamoja na dhana ya “kuishi duniani kwa kujilinda na vishawishi hatarishi vya kidunia” ikilenga kwamba Ibilisi hutumia fedha na mali za duniani kumtenganisha binadamu na Mungu kimahusiano; hiyo haina maana kwamba, binadamu anayemtegemea na kumwamini Mungu aache/ajitenge/asijihusishe na utafutaji na umilikaji wa mali pindi angalipo hapa duniani.

Hii ni kutokana na jinsi binadamu mwenyewe alivyoumbwa na Mungu. Suala la kumiliki mali ni la kimaumbile. Ni kama suala la ndoa. Ni la kimaumbile. Mungu amepiga marufuku matumizi ya tendo la ndoa kabla nan je ya ndoa lakini Mungu anatarajia binadamu kuoana kwa halali kwa sababu ni jambo la kimaumbile. Hali kadhalika na kumili uchumi. Mungu anamtarajia binadamu amtegemee, yaani atumie “imani yake kwa Mungu” kuanzia kubuni, kuzalisha, kuzidisha mali na kumiliki mali, na kuhakikisha anazitumia kwa ajili ya ufalme wa Mungu hapa duniani!

Kwa hiyo, mwaka huu 2016 ni fursa nyingine kwa kila binadamu anayemcha Mungu kutumia imani yake kwa Mungu kupokea na kutunza Baraka za kiuchumi kwa ajili ya ufalme wa Mungu hapa duniani. Mbaraka wa Mungu alioutamka kwa binadamu wa kwanza ulikuja kurejewa na Yesu Kristo pale aliposema “Tafute kwanza ufalme na hayo yote mtazidishiwa….” (MT.6:33) pamoja na “atapata mara mia katika ulimwengu huu wa sasa…” (MK.10:30)

Heri na Baraka za mwaka mpya kwa wote

SOMO: SIRI YA KIFO CHA GHAFLA (Mtu wa ndani "Roho") - ASKOFU GWAJIMA

$
0
0

Askofu Dkt: JOSEPHAT GWAJIMA
Somo: Siri ya kifo cha ghafla (Mtu wa ndani "Roho")

Sisi wito wetu ni kurudisha watu walioibiwa. Kwenye Biblia tumeona Elia alimfufua mtu, tumeona pia Elisha alimfufua mtoto, mifupa ya Elia ilimfufua mtu, Yesu Kristo mwenyewe Bwana wa wokovu wetu alimfufua binti Yairo,


Yairo alikuwa anamfuata Yesu siku nzima mpaka jioni, Bwana Yesu akamwambia Usiogope mwanao ataamka, tunajifunza kinyume cha Imani ni uoga, unapokuwa na uoga maana yake huna imani. Yesu alikuja duniani kufundisha wanafunzi wake ili watende kazi yake. Kijana kwenye lango la naimu aliyekuwa amebebwa kwenye jeneza alifufuliwa na Bwana Yesu. Siku moja Yesu alipelekewa taarifa kwamba Lazaro wa Bethania ni mgonjwa ila hakwenda bali alisubiria mpaka alipokufa akazikwa akakaa siku nne kaburini, watu walizomea sana wakacheka sana kwasababu Yesu alichelewa kufika lakini Yesu alikwenda akawaambia ndugu yao atafufuka na akawaambia wamwonyeshe walipomzika na waliondoe jiwe ndipo akamwita Lazaro njoo na hapo Lazaro akafufuka.

Yohana 5:25

Tunatakiwa tuingie kwenye ulimwengu wa rohoni kwa kushinda rohoni kwanza baadaye tushinde mwilini. kuna nguvu zinazofanya kazi rohoni unashindwa rohoni kwanza baadaye unashindwa mwilini, unapigwa rohoni kwanza baadaye unapigwa mwilini. Lakini Silaha za vita zetu zina uweza katika Mungu hata kuangusha ngome, ina maana zipo ngome kwenye familia zinazotakiwa kuangushwa, kuna ngome za laana, ngome za magonjwa, ngome za kushindwa zinazotakiwa kuangushwa kwa jina la Yesu.

Imeandikwa 2 Wakorintho 10: 3 "Maana ingawa tunaenenda katika mwili, hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili; (maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome;) tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu; na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo"

Waefeso 6; 12-17 Imeandikwa: "Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama.Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,na kufungiwa miguu utayari tupatao kwa Injili ya aman.Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu"

2 Wakorintho 4:9 Imeandikwa"Twaudhiwa, bali hatuachwi; twatupwa chini, bali hatuangamizwi"
Ulimwengu wa rohoni ni halisi kuliko ulimwengu wa mwilini mfano mzuri Kabla Yesu hajazaliwa alikuwepo katika ulimwengu wa rohoni na alikuwa anaitwa NENO, hata leo vyote vinafanyika kwa huyo na pasipo yeye hakuna kilichofanyika
Yohana 1;1-2 Imeandikwa: "Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu."

Isaya 41: 10 U"siogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu. Tazama, wote walioona hasira juu yako watatahayarika na kufadhaika; watu washindanao nawe watakuwa si kitu, na kuangamia. Utawatafuta wala hutawaona wale wapiganao nawe; watakuwa si kitu; watakuwa kama kitu kisichokuwa, wale waliofanya vita juu yako. Kwa maana mimi, Bwana, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia."

kuna wanaoshindana nawewe lakini watakuwa si kitu na wataangamia, sababu Bwana atakusaidia watakuwa kama kitu kisicho kuwa. Unatakiwa ufahamu kuwa wapo walioshindana na Bwana lakini hawakufanikiwa, wapo wafalme walioshindana na Bwana lakini hawakufanikiwa na utambue pia yeye ashindananaye na Bwana atapondwa kabisa. Usiogope hali uliyonayo. shetani anaogopesha ila yeye anaogopa kitu kimoja tu ambacho ni Neno la Mungu.

Ufunuo 19:13 Imeandikwa: "Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu."

Kuna ulimwengu wa rohoni na ulimwengu wa mwilini. unaweza kuhubiri maneno mazuri kwenye ulimwengu wa mwilini lakini usipo ugusa ulimwengu wa rohoni unakuwa hujafanya kitu.

Kwenye ulimwengu wa rohoni kufa sio kupotea, kuyeyuka wala kuzimia, Kufa ni kutoka nje ya mwili. Mwili ni kama nyumba ya mtu, na mtu anapotoka nje ya mwili anaitwa amekufa. Hakuna mtu ambaye aliwahi kukuona sababu unaonekana mtu wa nje ambaye ana kikomo chake hapa duniani (Udongo). Unaweza kuwa nje ya mwili watu wakasema umefariki na unaweza kuwa ndani ya mwili ukawa unaishi kwenye ulimwengu wa mwili.
Ukiwa nje ya mwili unakuwa mtu yuleyule, Gari haliwezi kwenda bila injini, vivyo hivyo mwili wako hauwezi kuishi bila wewe (roho) kuwepo ndani yake.

Roho ya mtu inapokuwa nje ya mwili tunasema mtu huyo amekufa, lakini ikiwa ndani ya mwili tunasema mtu huyo ni mzima. Mtu akifa anaingia kwenye raha ya ajabu hawezi kurudi kwa mapenzi yake mwenyewe labda Mungu awe na makusudi na mtu huyu kama hajamalizia kazi yake duniani.

Yohana 6:63 Imeandikwa "Roho ndiyo itiayo uzima, mwili haufai kitu; maneno hayo niliyowaambia ni roho, tena ni uzima."

2 wakorintho 12:2-5 Imeandikwa: "Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu. Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua); ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene. Kwa habari za mtu kama huyo nitajisifu; lakini kwa ajili ya nafsi yangu sitajisifu, isipokuwa katika habari ya udhaifu wangu."

Kile ambacho Biblia inasema kuhusu wewe ni ukweli kuhusu wewe lakini kile watu wasemacho kuhusu wewe sio ukweli kuhusu wewe, usiogope bali jiandae kwa mambo makubwa yajayo ambayo Mungu amekuandalia na usiogope kwa yanayokupata sasa hivi.

1 Yohana 4:2 Imeandikwa: "Katika hili mwamjua Roho wa Mungu; kila roho ikiriyo kwamba Yesu Kristo amekuja katika mwili yatokana na Mungu"

Yesu kristo ni Mungu aliyekuja duniani akavaa mwili akaishi kwetu kama mwanadamu akapigwa kama mwanadamu.

Stori kubwa kuliko zote duniani ni Mungu kuvaa mwili akawa kama mwanadamu.

2 Yohana 1: 7Imeandikwa: "Kwa maana wadanganyifu wengi wametokea duniani, wasiokiri ya kuwa Yesu Kristo yuaja katika mwili. Huyo ndiye yule mdanganyifu na mpinga Kristo."

Mathayo 27:50 Imeandikwa: "Naye Yesu akiisha kupaza sauti tena kwa nguvu, akaitoa roho yake."

Yesu aliamua kutoka ndani ya mwili wake akaenda chini kuzimu kule zilipokuwa roho za watu waliokufa kabla Yesu hajazaliwa. alipofika huko awatangazia kuwa yule waliyemsikia zamani kwamba ni nyoka wa shaba ndiye mimi, yule mliyekuwa mnamsiburia kwa hamu ndiye mimi nimekuja kuwachukua, na zamani kuzimu kulikuwa na sehemu mbili; za waliokufa watakatifu na wenye dhambi.

1Petro 3: 18 Imeandikwa: "Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa, ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri"

Mchawi ni nani?

Mchawi ni mtu yoyote (mtoto au mtu mzima) ambaye roho ya uchawi au jini wa uchawi linakaa ndani yake. Mchawi anapolala usiku, huamshwa na filimbi za kichawi ufikapo muda fulani maana wachawi nao wana filimbi zao "kama vile sisi tuliookoka tutakavyosikia parapanda ya Bwana Yesu atakapokuja kutuchukua" nao huamshwa kwa filimbi zao wanazozijua. Mtu huyu anapoamka Roho yake inatoka ndani ya mwili wake kwenda kuwanga/kuloga huku mwili wake unabaki nyumbani kwake ukiwa umelala.

kuna aina tofauti za uchawi
1. Kuna uchawi wa kurithishwa ambao mtu anaweza akawa ana roho ya uchawi amerithishwa lakini hajawahi kuutumia ama anautumia,
2. Kuna uchawi wa kununua ambao unanunuliwa kwa pesa nyingi.

Ayubu 4: 15 Imeandikwa: "Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu; Na nywele za mwili wangu zilisimama."

Kama ukifika mahali ukasikia nywele zinasimama fahamu mahali hapo kuna uchawi na mashetani na si uoga wa kawaida. Kama una nguvu za kushindana shindana nao lakini kama huna nguvu ondoka mahali hapo haraka, wachawi wapo na mchawi anaweza akawa mtu yeyote unayemtegemea na usiyemtegemea.

Wanyama wanaweza kuona "malaika" na wachawi.

Hesabu 22:23 Imeandikwa: "Na yule punda akamwona malaika wa Bwana amesimama njiani, na upanga wake mkononi mwake amekwisha kuufuta; punda akageuka upande ili kuiacha njia, akaingia shambani. Balaamu akampiga punda ili kumrejeza njiani."

Mungu anawapenda wanadamu wote.

Maombolezo 3:31 Imeandikwa: "Kwa kuwa Bwana hatamtupa mtu Hata milele."

Mungu hatesi Wanadamu na ukiwa unateseka sio Mungu anayekutesa, ukiwa unaumia sio Mungu anayekuumiza bali wapo wanaokuumiza na hao ndio unatakiwa uwashambulie kwa jina la Yesu.

Kabla huja lala tamka maneno ya mamlaka juu ya wachawi na yatatokea vilevile kama ulivyotamka kwa jina la Yesu. usipende kulala kabla hujatamka maneno, jifunze kutamka maneno kwa imani na mamlaka na Mungu atayajibu.

Wachawi wanaweza kutoka wakaingia ndani ya mtu na kunasa, wakiwa wametoka ndani ya mwili wao, wanaacha roho ya kichawi ili iweze kubakia na mwili wa mtu.

Ukiri:
"Kwa jina La Yesu kuanzia sasa ndugu, rafiki , jamaa ambaye alikuja kuniloga na kubakia ndani yangu ninaamuru ondoka kwa damu ya Yesu.".... shambulia kwa mamlaka ya jina la Yesu wachawi na mashetani yanayokusumbua kwa damu ya Mwanakondo na utakuwa huru kwa jina la Yesu.

BAADHI YA SHUHUDA BAADA YA MAOMBI YA ASKOFU MKUU Dr JOSEPHAT GWAJIMA.

Binti mmoja amefunguliwa baada ya maombi. Anasema alikuwa amelala usiku akaota nyoka mkubwa amekuja kumshika mguu alipojaribu kumkung'uta hakuondoka na akashtuka usingizini na kulala tena, Askofu alimwombea ili amwone aliyejibadilisha na kuvaa umbo la nyoka aliyemwona, ndipo akamwona rafiki yake aitwaye Rehema ambaye walikaa pamoja na kulala pamoja. Mungu amemfungua uoga na magonjwa aliyokuwa nao na kuwa huru.

Binti mmoja ameeleza alipokuwa mdogo kuna mama aliyekuwa jirani yake alikuwa hawezi kuuza ice cream bila kumpa yeye aiuze ya kwanza, ameelezea siku moja alikataa kuuza hizo ice cream ndipo alipolala usiku akawaona wazee wawili nditoni wanamwambia lazima awafuate na baada ya hapo akawa anakula mkaa sana, alipojaribu kuja kanisani alijiskia kifua kinabana sana lakini akajitahidi kuja ndipo akaombewa na Askofu na kufunguliwa kwa jina la Yesu na yule pepo wa kula mkaa akamtoka kwa jina la Yesu.

Binti mmoja aitwaye upendo ameeleza kuwa wakati wa usiku alikua hawezi kulala sababu kuna bibi wa kijijini kwao huwa anamtokea na kumwambia lazima aende naye na siku nyingine anamjia kama bibi wawili na mtoto mmoja wa kike au anakuja kwa umbo la nyoka. Wakati mwingine huwa analala kanisani na harudi nyumbani sababu ya uwoga wa huyo bibi anayemtokea. Binti huyo amewekwa huru kwa Damu ya Bwana Yesu na kuwa mzima.

SHUHUDA NI NYINGI SANA NA ZOTE ZINAPATIKANA KWA MFUMO WA DVD KANISANI UFUFUO NA UZIMA__UBUNGO__DAR ES SALAAM__TANZANIA.

WADAU WATAKA TAMASHA LA PASAKA LIVUKE MIPAKA

$
0
0


Na Mwandishi wetu.

Wadau na wapenzi wa muziki wa injili nchini, wametoa wito kwa waratibu wa tamasha la Muziki wa Injili la wakati wa Pasaka, Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, kuongeza wigo wa kufanyika katika nchi zote za Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa mmoja wa mashabiki wa Tamasha hilo linalobeba malengo ya kuutukuza ufalme wa Mungu na mengineyo ikiwemo kupata fedha za kusaidia makundi maalumu katika jamii, Anna Shibamla wa Yombo- Machimbo, jijini Dar es Salaam, anasema umefika wakati sasa tukio hilo likawa la nchi za Afrika Mashariki.

“Unajua Tamasha la Pasaka tayari lina sura ya kimataifa kwa sababu limekuwa likiwaleta pamoja waimbaji kutoka nchi mbalimbali, lakini kwa mawazo yangu umefika wakati sasa likawa linafanyika katika nchi za Afrika Mashariki ambazo ni Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi,” alisema Anna.

Anna aliyejitambulisha kama mmoja wa wadau wakubwa wa muziki wa injili na matamasha la Msama Promotions, alisema kwamba kama wazo hilo litafanyiwa kazi, kutalifanya tamasha lenyewe kuwa kubwa zaidi na kubeba maana zaidi kwani linaweza kuwa kielelezo cha umoja na nchi za Afrika Mashariki.

“Kwa mtazamo wangu, ni jambo linalowezekana kama waratibu watakuwa wamejipanga kwa mfano Tamasha la Pasaka likafanyika hapa jijini Dar es Salaam, kisha likaenda kutikisa Nairobi (Kenya); Kigali (Rwanda); Kampala (Uganda) na kule mjini Bujumbura (Burundi),” aliongeza.

Anna alisema kwa uzoefu wa zaidi ya miaka 16 wa Msama Promotions katika kuandaa tamasha hilo kwa ufanisi, anaamini anaweza kulifanya tukio hilo kuwa la Afrika Mashariki na likawa na mvuto wa aina yake huku likibeba uzito zaidi katika kutangaza ujumbe wa Neno la Mungu, amani na upendo kuanzia kwa watu hadi kwa nchi za ukanda huo.

Wazo hilo limeungwa mkono na Jasmin Jeremiah wa Ilonga Kilosa, Mkoani Morogoro kwa kusema hiyo itachangia kwa kiasi kikubwa waimbaji wa nchi moja kufahamika katika nchi zote za ukanda wa Afrika Mashariki, hivyo kuongeza wigo wa kupata soko la huduma yao ya uimbaji.

“Kama Tamasha la Pasaka litakuwa likifanyika katika nchi zaidi ya moja kwa mwaka, itawapa nafasi waimbaji kwa mfano wa Tanzania kujulikana katika nchi hizo kwa mfano Kenya, Rwanda na Burundi, hivyo sio tu kutaimarisha uhusiano kati ya nchi na nchi, pia itakuwa hivyo kwa waimbaji,” alisema Jasmine akiungwa mkono na Neema Gerald.

Neema alisema kitendo cha waimbaji wa nje kama Rebecca Malope wa Afrika Kusini ama Anastazia Mukabwa wa Kenya wakaenda kushiriki katika Tamasha la Pasaka nchini Rwanda au Burundi, kutaleta mvuto zaidi wa tukio hilo na kusema anaunga mkono suala hilo kwa asilimia 100.

Wazo hilo la wadau ni kutokana na tamasha hilo lililoasisiwa tangu mwaka 2000, ambalo limekuwa likifanyika nchini kwa kuanzia jijini Dar es Salaam na katika mikoa kadhaa, hivyo maoni ya wadau ni tukio hilo kwenda mbali zaidi ya hapo kwamba liwe linafanyika katika nchi zaidi ya moja katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Alipotafutwa kuhusu maoni hayo ya wadau, Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizii ya Tamasha hilo, Alex Msama, alisema ni wazo zuri kwani huduma na malengo yake vitazidi kupanuka na kubeba sura ya kimataifa zaidi ikiwemo kuwa kielelezo cha umoja na mshikamano wa nchi za Afrika Mashariki na kuongeza wataketi kutafakari suala hilo.

SHANGWE ZA GK: NI ZAMU YA RUTH NA EDSON MWASABWITE

$
0
0

Hayawi hayawi sasa yamekuwa, tarehe 3 Januari ndio siku ambayo historia ya Edson na Ruth imeandikwa kwenye Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Kijitonyama na kisha sherehe kufanyika kwenye ukumbi wa Khana Khazana uliopo Victoria Jijini Dar es Salaam, kuanzia saa mbili hadi saa tano usiku.

Tukio hilo la kipekee liliongozwa na MC Msomi wa sanaa ya mawasiliano, Lawrence Mwantimwa, amabapo pia Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, CHAMUITA, kikiongozwa na Rais wao, Addo November kilikuwepo kuhakikisha kwamba sifa na utukufu zinamrudia Mungu kupitia uimbaji.

Katika hafla hiyo ambayo ilidhaminiwa na Mwanti Car Trade na Gospel Kitaa, Edson Zako Mwasabwite aliimba wimbo maalumu wa kumshukuru Mungu, aliyemuwezesha kufika siku hiyo.

Christopher Mwahangila
Wenyeji, Ruth na Edson
MC Lawrence naye akaimba
Lilian Kimola





Addo November























Ni kama vile Makondoeko ndiye bodyguard, huku Faraja naye akiwa mpambe wake. Ilipendeza siku hiyo.

Gospel Kitaa inawatakia maisha mema maharusi, waishi katika utukufu wa Mungu.

SHANGWE ZA GK: SHEREHE YA SIKU YA KUZALIWA KWA ELIAZER KIMOLA

$
0
0

Siku na masaa zinasonga, na utukufu unazidi kumrudia Mungu. Tarehe 7 ikawa kumbukumbu ya siku ya kuzaliwa kwa Eliazer Kimola ambaye ametimiza miaka 7 ya kuzaliwa. GK ilifanikiwa kufika na kuungana na watoto wenzake kwa pamoja katika kukamilisha siku hii muhimu lililofanyika KFC Mikocheni Jijini Dar es Salaam.

Zifuatazo ni picha za tukio;



MC King Nyorobi katika kuhakikisha kila kitu kiko sawia.

Mtu na rafikize



Kuku ni kwa tumbo


Big bro na madogo





Mama na watoto














Team marekebisho


Kata keki tule



Edna Kuja naye aliambatana na watoto wake.

mahesabu yanapigwa

equation imebalance, kazi na ianze





Sijui kama wanacheza step ama wanfanya mazoezi kabla ya msosi... sijui


Anaitwa Precious Kimola



Ujumbe kutoka kwa mama yake;

Tarehe 7 January mwaka huooo Mungu alitupa wewe kama zawadi ya mtoto wa kwanza mikononi mwetu. Akatuongoza kukulea na kukutunza tukiwa hatujui kabisa mazoezi haya ya vitendo...
My son ulikuwa kibonge kweli kuliko mimi mama yako wengine hawakuamini kama ni kweli mimi mama yako....ubonge huo ulinifanya mama yako nionekane naweza kweli kulea ki ukweli ni Mungu tu aliyafunika hayo...Leo ni tar 7 ni miaka 7 ulizaliwa jumatano ukazunguka hadi ukaifika hiyo jumatano, maana ya 7 ni utimilifu...na leo ni alhamis umeanza mzunguko mwingine mpya katika maisha yako....Nakupenda sana mwanangu Mungu alikuumba kwa kusudi na tumekuwa tukikuambia mimi na baba yako...uyashike sana mausia yetu mwanangu Eliazer ndipo utaishi miaka mingi na kustawi sana...

Nakupenda mno wewe wajua.....
Happy 7th birthday my son Eliazer!

NIKUFANANISHE NA NANI NDIO CHAGUO LA GK, NI VIWANGO MKOANI

$
0
0


Jumapili ya pili kwa mwaka 2016 tunaendelea kumshukuru Mungu kwa uzima na nafasi yakuwepo kwetu kwa mwaka huu, GK imekuchagulia wimbo kutoka kwaya Uinjilisti Uyole ya jijini Mbeya chini ya kanisa la Kilutheri wakiwa wameshirikisha mwimbaji maarufu aliyetamba na kwaya ya uinjilisti Kijitonyama ya jijini Dar es salaam Modest Morgan. Wanakwambia 'Nikufananishe na nani'.

Ni uhakika kwamba utabarikiwa na waimbaji hawa hususani ujumbe uliopo kwenye wimbo husika na namna mwanzishaji alivyoweza kuimbisha vyema na kuiongoza kwaya kufikisha ujumbe huu wa kumwabudu na kumsifu Mungu. Tunawatakia jumapili njema

SOMO: MUNGU ANATEGEMEA UZAE ZABIBU NZURI,JE UNAZAA NINI?

$
0
0

Na King Sam

SHALOM
KWA SABABU YA KUKOSA MAARIFA UMECHUKULIWA MATEKA HUZAI KAMA MUNGU ALIVYOTEGEMEA UZAE,
WEWE NI SHAMBA LA MUNGU LA MZABIBU MUNGU ANATEGEMEA UZAE MZABIBU MZURI,JE UNAZAA NINI?

Isaya Isaiah 5:1-13
Na nimwimbie mpenzi wangu wimbo wa mpenzi wangu katika habari za shamba lake la mizabibu. Mpenzi wangu alikuwa na shamba la mizabibu, Kilimani penye kuzaa sana;
Akafanya handaki kulizunguka pande zote, Akatoa mawe yake, Akapanda ndani yake mzabibu ulio mzuri, Akajenga mnara katikati yake, Akachimba shinikizo ndani yake; Akatumaini ya kuwa utazaa zabibu, Nao ukazaa zabibu-mwitu.
Na sasa, enyi wenyeji wa Yerusalemu, nanyi watu wa Yuda, amueni, nawasihi, kati ya mimi na shamba langu la mizabibu.
Je! Ni kazi gani iliyoweza kutendeka ndani ya shamba langu la mizabibu nisiyoitenda? Basi, nilipotumaini ya kuwa litazaa zabibu, mbona lilizaa zabibu-mwitu?
Haya basi, sasa nitawaambieni nitakalolitenda shamba langu la mizabibu; nitaondoa kitalu chake, nalo litaliwa; nitabomoa ukuta wake, nalo litakanyagwa;
nami nitaliharibu; wala halitapogolewa wala kulimwa, bali litamea mbigili na miiba; nami nitayaamuru mawingu yasinyeshe mvua juu yake.

Kwa maana shamba la mizabibu la BWANA wa majeshi ndilo nyumba ya Israeli, na watu wa Yuda ni mche wake wa kupendeza; akatumaini kuona hukumu ya haki, na kumbe! Aliona dhuluma; alitumaini kuona haki, na kumbe! Alisikia kilio.
Ole wao waongezao nyumba baada ya nyumba, na kuweka shamba karibu na shamba, hata hapana nafasi tena, nanyi hamna budi kukaa peke yenu kati ya nchi!

BWANA wa majeshi asema katika masikio yangu, Hakika majumba mengi yatakuwa ukiwa, naam, majumba makubwa, mazuri, yatakuwa hayana watu.
Kwa maana shamba la mizabibu la eka kumi litatoa bathi moja tu, na homeri ya mbegu itatoa efa tu.
Ole wao waamkao asubuhi na mapema, wapate kufuata kileo; wakishinda sana hata usiku wa manane mpaka mvinyo imewaka kama moto ndani yao!
Na kinubi, na zeze, na matari, na filimbi, na mvinyo, zote ziko katika karamu zao; lakini hawaiangalii kazi ya BWANA wala kuyafikiri matendo ya mikono yake.

Kwa sababu hiyo watu wangu wamechukuliwa mateka, kwa kukosa kuwa na maarifa; na watu wao wenye cheo wana njaa, na wengi wao waona kiu sana.

YESU ALISEMA HAYA MANENO NA HAKUNA NENO LILILOSEMWA NA YESU HALITATIMIA YOTE YATATIMIA YOTE,

Yohane John 15:1
Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.
2 Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.
3 Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.
4 Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.
5 Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.
6 Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.
7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

YESU ALIKUJA KUKAMILISHA PALE MSALABANI ILI WEWE USIFE NA MAGONJWA USIFE MASIKINI USIFE KWA UCHAWE USIFE KWA AJALI USIFE KWA KUJINYONGA USIFE KWA SUMU USIFE KWA NJAA HIVI VIFO NI KAZI YA SHETANI NA SI KAZI YA MUNGU,
KILE UNACHOZAA NDICHO KINALETA MATOKE KATIKA MAISHA YAKO,
POKEA NEEMA YA YESU YA KUUZA MZABIBU MWEMA ILI UWE NA MATOKEO YA KIMUNGU KATIKA MAISHA YAKO,AMEN

KIGOMA WALITAKA TAMASHA LA PASAKA

$
0
0
Mwisho wa reli, Kigoma. ©Mapio
Na Mwandishi Wetu

Wadau wa Tamasha la Pasaka mkoa wa Kigoma wameonesha nia ya kulitaka Tamasha la Pasaka mwaka huu ili kuepusha vurugu zinazoendelea kwa majirani zao Burundi.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya wakazi hao wanasema kwa kuwa Tamasha hilo ndio mkombozi wa nchi za Afrika Mashariki hasa kwa masuala ya amani.

Wakazi hao wameiomba Kampuni ya Msama Promotions ya jijini Dar es Salaam, kulipeleka tamasha hilo mkoani humo kwa sababu majirani zao nchi ya Burundi wanahitaji uponyaji kutoka kwa waimbaji wa nyimbo za injili na viongozi wa dini.

Burundi imekumbwa na machafuko yaliyotokana na kupinga uongozi wa awamu ya tatu wa rais Pierre Nkurunzinza ambako kila kukicha nchi hiyo inapoteza idadi kubwa ya wakazi wake kwa sababu ya vita.

Ngobho Nyobho mkazi wa Kasulu mkoani humo anasema, tamasha hilo Mkoani Kigoma litakuwa kichocheo cha kuondosha machafuko yanayoendelea nchini humo hasa kwa mauaji ambayo yanawamaliza wananchi wa nchi hiyo kila kukicha.

Mkazi huyo alisema kwa kuwa Tanzania ndio kisiwa cha amani ambayo iliasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, ambako nchi jirani ambazo zinakosa amani hukimbilia Tanzania kwa lengo la kujiweka sawa.

“Tanzania ni nchi ambayo inasifa kubwa ya kuwa na amani ambayo, nchi zingine zinazoizunguka hakuna, kila kukicha watu wanauana kwa sababu mbalimbali, tunawaomba waandaaji wa Tamasha la Pasaka, kampuni ya Msama Promotions kulifikisha mkoani kwetu kwa sababu ya kuwaomba jirani zao kuacha vita inayoendelea,” alisema.

Naye Ndinda Mahiri mkazi wa Kiganza mkoani humo alisema jirani zetu wanahiaji uponyaji kutoka kwa waimbaji wa Injili na viongozi wengine wa dini na wakemee machafuko yanayoendelea kwa jirani zetu.

Mkazi huyo alisema Kampuni ya Msama Promotions iwafikirie na wao kwa sababu wako karibu na Burundi ambako kuna machafuko yanayoendelea kumaliza idadi kubwa ya wananchi wa nchi hiyo.

Naye Mkurugenzi wa Msama Promotions, Alex Msama alisema kamati yake imelipokea ombi hiloambako wameahidi kulifanyia kazi ili majirani zetu Bueundi watapata uponyaji kutoka kwa Mungu kupitia waimbaji wa nyimbo za Injili na viongozi wa dini.

HOJA: MAOMBI NA CHANGAMOTO ZAKE

$
0
0
Askofu Sylvester Gamanywa,
WAPO Mission International.

©Daily Prayer US
Kama ilivyo kawaida katika mwanzo wa mwaka mpya, suala la maombi lazima lipewe kipaumbele kwa kila mwamini kwa sababu Ukristo umesimama katika maombi na Neno la Kristo. Leo nataka kudokeza vipengele muhimu juu ya dhana nzima kuhusu maombi. Biblia imeandika taarifa kuhusu maombi zaidi ya mara 138. AK mara 78 na AJ mara 53 na Yesu mwenye ametaja neno maombi mara 15 katika AJ. Pamoja na ushahidi wa kimaandiko katika Biblia lakini uzoefu unaonesha Maombi yana changamoto nyingi na baadhi yake nitazijadili  katika hoja hii. Nitawasilisha kwa mtindo wa maswali na majibu:

Kwanini kuomba ni lazima?

Kuna sababu nyingi za kibiblia lakini nizitaje 2 muhimu kwa mujibu wa somo la leo. Sababu ya kwanza ni “Agizo la Mungu la kuwasiliana na yeye” kwa ajili ya kudumisha ushirika na Mungu. Hili ndilo kusudi la msingi la kumuumba binadamu. Kuwa na ushirika naye. Hakuna ushirika pasipo mawasiliano.

Kabla ya anguko la binadamu wa kwanza, Mungu alikuwa na kanuni ya kukutana na alasiri na Adamu na Eva na kuzungumuza nao. Itakumbukwa pia siku binadamu alipoanguka dhambini bado Mungu alimfuata wakafanya mawasiliano. Kitabu cha Mwanzo sura nzima ya tatu inaonesha mawasiliano ya mwisho kati ya Mungu na binadamu kabla ya kufukuzwa kutoka Bustani ya Edeni

Sababu ya pili kwanini kuomba ni lazima ni “Binadamu kumtegemea Mungu 100%”!Kwa asili binadamu aliumbwa kufanya mambo yote kwa uongozi wa Mungu na sio kujifanyia maamuzi yake kivyake vyake. Mungu anataka tumtegemee yeye kwa kila jambo, liwe kubwa au dogo.

Na njia pekee ya kumwonyesha kwamba tunamtegemea ni sala. Kumshirikisha, kutafuta kujua mapenzi yake ni nini, kufanya maamuzi yatokanayo na maagizo yake, yote yanaashiria “kumtegemea Mungu 100%.

Tunajifunza ukweli huu kutoka kwa Yesu mwenyewe ambaye hakufanya jambo lolote ambalo hakuagizwa na Baba yake. Ndiyo maana kila mara alikuwa na vipindi vyake vya kuomba akiwasiliana na Baba yake kwa ajili ya kudumisha USHIRIKA PAMOJA NAYE na pia kwa ajili ya KUTAFUTA UONGOZI WA BABA 100% kwa utumishi wake duniani.

Na ndiyo maana akawaagiza wanafunzi wake kuendelea tabia ya maombi kwa sababu ni kwa njia hiyo hiyo wangedumisha USHIRIKA pamoja naye akiwa mbinguni na pia kupata uongozi wake kwa ajili ya utumishi.

Mwisho kabisa ndiyo maana alimtuma Roho Mtakatifu aje kufanya makazi ndani yao pamoja na wote watakaompokea Yesu kupitia injili yao; ili zoezi la kuwasiliana na Mungu liwe endelevu na lenye tija.

Kwanini kuomba ni kitu
kigumu kwa wengi?

Pamoja na kwamba, maombi ni muhimu sana kwa kila mwamini anayemfuata Yesu Kristo, pamona kwamba kila mtu angependa kuwasiliana na Mungu mara kwa mara ili kujenga uhusiano imara na Kristo; ni jambo la kushangaza sana kuona kwamba “kuomba” kimmekuwa kitu kigumu kutekelezeka kwa walio wengi.

Sala nyingi zinanzofanyika ni zile ambazo hazina tija na za maigizo tu ya kukariri ili kuridhisha nafsi kwamba ni ibada. Lakini hazina matokeo yoyote na wanaosali hata kama naafsi zao kwa ndani zinapenda lakini uhalisia ni kuwa hawajisikii kuwa na uhusiano wowote wa karibu na Mungu.

Haya, hivi ni kwanini kuomba ni kitu kigumu namna hii? Imenichukua muda mrefu kutafakari, nikianza na changamoto ninazopambana nazo mimi mwenyewe katika zoezi hili la kiroho, na kasha kujifunza kwa wakristo wenzangu wengine, hasa wale walionitangulia katika mambo ya imani na utumishi huu. Bado nimegundua kwamba, hakuna bingwa wa kujibu swali hili kwa ujasiri.

Ni kutokana na uzito, au unyeti wa changamoto hii ya “kushindwa kuomba” wakati hii ndiyo njia pekee ya kufanikiwa kiroho na kimaisha. Majibu yangu yaweza yasiwe ndio mwisho wa yote; lakini nina imani yatasaidia kuutafakari ukweli kwa jicho la maandiko matakatifu na bila shaka ufumbuzi ukaanzia hapo.

Kuna vikwazo vikubwa viwili vinavyokwamisha waamini kumwomba Mungu. Cha kwanza ni “Udhaifu wa mwili”! Hii ni kwa mujibu wa Yesu Kristo alipowaambia wanafunzi wake akisema: “Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni; roho i radhi, lakini mwili ni dhaifu.” (MT.26:41)

Kumbuka kisa cha wanafunzi kushindwa kuomba pamoja na Yesu, wakazidiwa na usingizi wakalala badala ya kukesha wakiomba. Mara tatu Yesu alikuwa akija kuwaamsha ili waombe na akiondoka wanalala usingizi.

Yesu akasema, “mwili ni dhaifu”! Tendo la kuomba ni la kiroho. Na roho ya binadamu ambaye asili yake ni kutoka kwa MUngu ndiyo ina shauku ya kuomba. Lakini mwili asili yake ni udongo hautaki mambo ya kiroho. Ndiyo maana umekataliwa kwamba “hautaingia mbinguni” Kwa hiyo. Mwili unatumiwa sana na nguvu za Ibilisi kuleta mgomo dhidi ya tendo la kuomba.

Ufumbuzi wa tatizo hili, ni zoezi la kujikana kweli kweli na kuutiisha mwili ukubali kutumika kuomba, Maana kimaumbile roho zetu haziwezi kuomba pasipo mwili kushiriki kwa sababu wenyewe ndio umeshikilia mifumo ya mawasiliano. Kwa hiyo, tujue kwamba, kamwe mwili kwa asili hauwezi kutuhamasisha sisi kuomba, wala haupendi sisi tuombe, kwa sababu wenyewe hauna faida na hayo yajayo katika ulimwengu wa roho.

Kikwazo kingine kinachozuia wengi kutokuomba ni “kutokujua kuomba ipasavyo”! Hii tunafundishwa na Mtume Paulo pale alipowaandikia warumi akisema: “ Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.” (Rum.8:26)

Hapa kuna mchanganyiko wa mambo mengi yenye kuhitaji maelezo ya kina. Kwanza tunaona habari ya msamiati wa “udhaifu wetu”….. tunao udhaifu wetu katika suala la kuomba, na udhaifu wenyewe ni kuwa “hatujui kuomba itupasavyo…” Maana yake tunatumia akili na hisia zetu kuomba vitu ambavyo sio kipaumbele kwa Mungu, au tunaomba huku tumeathiriwa na shida na matatizo au masukosuko au msongo wa mawazo na kudhani kwamba hayo ndiyo mahitaji yetu mbele za Mungu.

Yote hayo ni “udhaifu wa kutokujua kuomba itupasavyo” Sasa ufumbuzi wa tatizo hili ndiyo maana Yesu akamruhusu Roho Mtakatifu ashuke na kufanya makazi ndani yetu ili yeye ndiye ashike hatamu za kuomba kwa niaba yetu.

Nafasi ya imani katika maombi

“Kwa sababu hiyo nawaambia, yoyote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” (MK.11:24)

Haya tayari tumejifunza umuhimu wa maombi na vikwazo vyake na hapa nataka tujifunze kuhusu nafasi ya imani katika maombi. Tukichukulia mfano wa kibinadamu tu ambapo mtu anaondoka kwenda kukopa fedha kwa mtu mwingine. Sasa mpaka hapa baadhi yetu tunanweza kuw hatujui kwamba, mpaka mtu achukue hatua ya kumwendea mtu, “tayari amekwisha kumwamini mtu huyo moyoni kwamba, anazo fedha na kwamba atakubali kumkopesha tu.” 

Na sababu za kumwamini zaweza kuwa ni uwezo wa kifedha aliona nao mhusika, na uhusiano wa karibu walio nao baina yao.

Na hata ikitokea mtu akakosa kupata mkopo kutoka kwa huyo mtazamo wake juu ya mtu huyo haubadiliki. Anajua ameamua kutokumkopesha tu amekataa au amemnyima nk. Lakini haamini kwamba hana uwezo na kwamba hawana mahusiano mabaya kiasi cha kumtokubali kumkopesha.

Mpendwa msikilizaji, kama waamini tungefanikiwa kumwamini Mungu angalau kwa kiwango hiki kila tunapoamua kumpelekea mahitaji yetu, bila shaka tungepata mrejesho wa kushangaza kutoka kwa Mungu!

Hivi unajua kwamba “Imani ni mtazamo na nia juu ya Mungu” Mungu anasema kwamba “kila amwendeaye yeye lazima aamini kwamba yuko, na kwamba huwapa thawabu wamtafuato.” (HBR.11:6)

Wengine wetu tunapomwendea Mungu huwa hatuna uhakika 100% kwamba tutapata yale tunayokwenda kumwomba. Tunahisi kwamba, yeye ni mkali sana mtakatifu sana kiasi kwamba hata kutusikiliza hajali hasa tunapokuwa tumemkosea kwenye mambo Fulani Fulani. Mtazamo wa jinsi hii unatufanya tuwe na picha tofauti na Mungu alivyo kwetu!

Mungu kwetu ni Baba na ni zaidi ya baba wa kidunia. Amekwisha kuweka kila hitaji letu sawa sawa na anachosubiri ni sisi wenyewe kumwendea kwa shauku tukijua kwamba yeye ni mwaminifu kwa ahadi zake na kamwe hawezi kutuangusha. Ni kufuru kumwamini binadamu kuliko Mungu.

Mwisho.

TANZIA : BAHATI BUKUKU AFIWA NA MAMA YAKE MZAZI JIJINI MBEYA

$
0
0


Muimbaji wa nyimbo za injili Bahati Bukuku amefiwa na mama yake mzazi ambaye amefariki Jana usiku wa January 11 2016.

Umauti umemfika mama mzazi wa muimbaji huyo huko mkoani Mbeya ambapo alikuwa akiuguzwa maradhi ya Moyo.

Kwa upande wake Bahati Bukuku yupo njiani kuelekea Mbeya kwa ajili ya msiba huo ambao upo Mwanjelwa. Taarifa zaidi zitakujia kwakadri ambavyo tutakuwa tukizipata.

Mungu azidi kumtia Nguvu na kumfariji Bahati Bukuku pamoja na familia yake kwa ujumla.

    BWANA AMETOA NA BWANA AMETWAA, JINA LA BWANA LIHIMIDIWE.

CAMPUS NIGHT ARUSHA NI IJUMAA HII TAREHE 15

$
0
0
Zikiwa zimebakia siku mbili kulekea mkesha wa Campus Night 2016 pale SheikAmri Abeid Karume jijini Arusha ambalo limeandaliwa na Manna Tabernacle Bible Church (MTBC) - Moshi tarehe 15 januari mwaka huu kuanzia saa mbili usiku,tayari jukwaa limeshaanza kufungwa katika katika huo.

fb/John Pazia
 
fb/John Pazia

Tukio hilo itahusisha waimbaji mbali mbali wa muziki wa injili kama Angel Benard,Paul Clement, MTBC Praise Team,VOT,Abenego & The Worshipers na wengine wengi,Ambapowahudumu wakiwa ni Mchungaji Dickson Mtalitinya(mwenyeji) pamoja na Martin & Jannekah Gooya(nairobi).
 

SOMO: KARAMA ZA ROHO MTAKATIFU (1 & 2) - MCHUNGAJI MADUMLA

$
0
0









Bwana Yesu asifiwe…

Si watu wengi wenye kujua maana halisi ya Karama maana wapo watu wenye kulichanganya neno hili na neno kipaji. Kipaji na karama ni maneno mawili tofauti kabisa kwa sababu kipaji ni uwezo wa asili wa kimwili ndani ya mtu wa kutenda jambo fulani ,bali karama ni uwezo wa kiroho wa kutenda sawa sawa na muongozo wa Roho mtakatifu.

Hivyo basi,

Karama ni utendaji kazi wa Roho mtakatifu ndani ya mwamini aliyeokoka.

Kila aliyeokoka amepewa karama fulani kwa kufaidiana katika kuujenga mwili wa Kristo.

Katika fundisho hili zuri,tutajifunza katika vipengele vifuatavyo;

01. Tofauti kati ya ujuzi,kipaji na karama.

02. Tofauti kati ya wito na karama.

03.Aina za karama za Roho mtakatifu.

04. Sifa kuu za karama za Roho mtakatifu.

05. Faida za karama za Roho mtakatifu.

06. Utawezaje kuitambua karama yako?

07. Ni namna gani utachochea karama yako?

08. Ni kwa namna gani karama yangu itampendeza Mungu?

09.Changamoto za utendaji kazi katika kila karama.

01.TOFAUTI KATI YA UJUZI,KIPAJI NA KARAMA.

A)Ujuzi.(Skill)

Ni uwezo upatikanao kwa njia ya elimu fulani. Uwezo huu umuwezesha mtu kutenda au kufanya jambo fulani kwa sababu ya elimu aliyoipata.

Hivyo,UJUZI ni uwezo wa kufanya jambo fulani katika ubora,au katika ufundi fulani kwa sababu ujuzi huo umepatikana kwa kusomea au kujifunza ( Capacity to do something well; technique, ability. Skills are usually acquired or learned, as opposed to abilities, which are often thought of as innate.)

Mfano 01; Mtu anaweza akaenda kusomea ufundi magari,kisha baadaye akawa ni fundi mzuri sana wa kutengeneza magari na hata kuyarekebisha. Ufundi huu uliopatikana kwa kisomo au mafunzo fulani ni ujuzi.

~Ujuzi hauji automatically yaani haumjii mtu moja kwa moja bali ni lazima akajifunze kwanza ndiposa awe mjuzi wa jambo fulani.

Mfano 02. Katika biblia tunaona wapo watu wengi tu waliokuwa na ujuzi wa kufanya mambo tofauti tofauti,mfano tunasoma; “ Ada akamzaa Yabali; huyo ndiye baba yao wakaao katika hema na kufuga wanyama.Na jina la nduguye aliitwa Yubali; huyo ndiye baba yao wapigao kinubi na filimbi.“Mwanzo 4:20-21

Yabali baba yao,bila shaka alipitisha elimu juu ya ufugaji wanyama. Elimu hii juu ya ufugaji ilikuwa ni ujuzi wa namna ya kufuga wanyama. Katika jamii ya kiyahudi kulikuwepo namna ya kurithisha elimu ya ufugaji kutoka jamii moja hadi jamii nyingine. Mtazame pia Yubali baba yao wapigao kinubi na filimbi. Bila shaka elimu ya namna ya kupiga kinubi na filimbi ilifundishwa na kurithishwa. Na jambo hili tunaliona hadi katika kizazi cha Daudi,Daudi alikuwa ni mpigaji mzuri wa kinubi. Imeandikwa;

“Ikawa siku ya pili yake, roho mbaya kutoka kwa Mungu ikamjilia Sauli kwa nguvu, naye akatabiri ndani ya nyumba. Basi Daudi alikuwa akipiga kinubi kwa mkono wake kama siku zote; naye Sauli alikuwa na mkuki mkononi mwake.” 1 Samweli 18:10

Ukijaribu kuyatizama maisha ya baadhi ya wanafunzi wa Yesu,wengi wao walikuwa na ujuzi fulani katika maisha yao kabla ya kuitwa kuwa mitume. Mfano Petro alikuwa ni mvuvi,uvuvi huu wa Petro ulitokana na elimu ya awali kutoka kwa baba yake na jamii yake iliyokuwa wavuvi tangu awali. Alikadhalika ukimtazama mwinjilisti LUKA alikuwa na ujuzi mzuri tu wa utabibu kabla ya kuokoka katika misafara ya mtume Paulo. Tazama Wakolosai 4:14

▪Je ujuzi unahitajika katika kanisa la leo?

JIBU;Ujuzi unahitajika sana katika kanisa la leo. Maana si wote watakaokuwa ni wachungaji au si wote watakao kuwa ni waalimu kanisani bali wapo wengine watakaokuwa ni waamini wenye ujuzi wa mambo fulani yenye kulifaa kanisa liweze kusonga mbele kwa kujitosheleza. Mfano; Kanisa linahitaji wataalamu waliosomea namna ya kuendesha kitengo cha utawala ( Management) yaani jinsi ya kukontroo/ku-control matumizi ya pesa,jinsi ya kuwa na miladi endelevu ya kanisa,jinsi ya kuandaa mikutano,seminas,makongamano ( Maana huduma hizo zote zinahitaji pesa)

Tuangalie kanisa la kwanza lilivyoweza kushughulikia suala hili la utawala, ;

“Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manung’uniko ya Wayahudi wa Kiyunani juu ya Waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku.Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani

Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili;na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile Neno.” Matendo 6:1-4

Hapo,tunaona kabisa mitume walibidi waweke mambo ya kiutawala(management) ili kukidhi mahitaji ya kila siku ya watu wote. Kipindi mitume wanahudumu mezani pa Bwana,hapo ndipo pakatokea hali ya kutokutenda sawa kwa baadhi ya wajane wa kiebrania kusahauliwa katika huduma ya kila siku. Kumbe basi kanisa likikosa utawala(management team) halitaweza kutenda haki. Lakini pia kanisa la namna hii linaweza likakumbwa na manung’uniko mengi ya kihuduma za kila siku,maana wapo watu ambao watasahaulika katika baadhi ya mambo mbali mbali.

Kumbuka,Kazi ya utawala sio kazi ya mchungaji hapo kanisani kwa sababu kazi ya mchungaji ni kulihudumia lile neno na kuomba (Matendo 6:3-4).

Hivyo basi ,ujuzi unahitajika sana katika kanisa la leo,kumbuka tena watu wa utawala ni lazima wawe na ujuzi wa kuendesha mambo kanisani pasipo upendeleo wowote ule.

Lakini pia watu hawa wenye ujuzi wanatakiwa wawe ni watu safi rohoni,wasiwe na mawaa maana ikiwa watakuwa ni watu ovyo,yaani hawajaokoka wakamaanisha~basi waweza wakapendelea baadhi ya waamini hata kama wamejawa na ujuzi wa kutenda mambo. Tazama mfano wa wale saba waliochaguliwa katika kuongoza mambo ya utawala katika kanisa la kwanza (Matendo 6:3),Watu hawa walikuwa ni watu wema waliojawa na Roho mtakatifu…

(B) Kipaji (Talent)

~Ni uwezo wa kiasili (wa kuzaliwa nao) wa kimwili wa kutenda jambo au kitu fulani pasipo kujifunza. (Natural ability or skill)

Mungu ametoa vipaji mbali mbali kwa watu wake. Mfano,wengine wamepewa wawe waimbaji,wengine mafundi,wengine wachoraji,wengine wacheza sarakasi N.K Mara nyingi vipaji hivi hutumika kama sehemu ya kujiingizia kipato kwa mwenye nacho.

Maana wapo watu ambao ni mafundi wazuri wa mambo mbali mbali mfano fundi radio,ambaye kwa kweli hajasomea ufundi radio bali amezaliwa na uwezo wa kukorokochoa radio yoyote na kisha kugundua tatizo pamoja na kupata uvumbuzi wake,kisha na kujipatia kipato chake kwa ufundi huo. Wengine utakuta ni wachoraji wazuri sana,uwezo wa kuchora pasipo kujifunza mahali popote pale ni kipaji,ambapo kipaji hiki kinatoa kipato.

Ujuzi unatofautiana na kipaji,kwa maana ujuzi unaupata kwa sababu ya elimu fulani uliyoipata darasani wakati kipaji ni uwezo wa kuzaliwa nao wa kutenda jambo pasipo kujifunza darasani. ( Ingawa mtu anaweza akawa ni fundi radio kwa kusomea,ufundi huu ni ujuzi.)

Lakini kumbuka hili; Mwenye kipaji anaweza akaenda shule kwa madhumuni ya kukikuza kipaji chake. Na hapo,ndiposa kipaji kinakuwa kina mapana makubwa ya utendaji kazi.

Je kipaji kinahitajika katika kanisa la leo?

JIBU;

Kipaji kinahitajika sana katika kanisa la leo sababu watu hawa wenye vipaji wanaweza kutumika kama chachu ya kuwakusanya watu wengi sehemu moja,kisha baada ya hapo wakahubiriwa na muhubiri na hatimaye kuvuna roho za watu hao.

Mfano;Wenye vipaji vya uchezaji,wanaweza wakacheza mahali pa mkutano wa injili kabla ya muhubiri kupanda,gafla waweza kuona kundi kubwa la watu wakitekewa na machezo ya nyimbo za sifa kwa Bwana kupitia wale wenye vipaji vya kucheza,kisha katika hali hiyo hiyo ndiposa muhubiri aja kuzikomboa roho za watu wale waliokusanyika. Mfano huu mimi ninaufananisha na mvuvi aliyezitega nyavu zake baharini kisha samaki kunaswa na zile nyavu zake.

Kumbuka;kipaji ni zawadi ya bure itolewayo na Bwana Mungu kwa watu bila kuzingatia itikadi za imani zao. Maana mtu anaweza akawa hata aamini kabisa!yaani mpagani lakini akawa bado ana kipaji kizuri tu cha kufanya jambo fulani,Tofauti na karama,maana karama inamtaka mtu aokoke kwanza.

C)Karama(Spiritual gift)

Ni utendaji kazi wa Roho mtakatifu ndani ya mwamini aliyeokoka.

Zifuatazo ni baadhi ya tofauti chache kati ya ujuzi,kipaji na karama;

(i)Ujuzi ni uwezo upatikanao darasani,kipaji ni uwezo wa kuzaliwa,karama ni uwezo wa Roho mtakatifu wa utendaji kazi baada ya kuokoka.

(ii)Ujuzi ni kwa kila atakayesomea,kipaji ni kwa kila mtu sawa sawa na alichopewa,karama ni watu wachache waliokoka kwanza na kudumu katika wokovu.

(iii) Ujuzi una gharama ya pesa katika upatikanaji wake,kipaji hakina gharama ya pesa maana mtu hawezi kununua kipaji kwa pesa,karama ina gharama ya kuyauza maisha yako kwa Bwana Yesu ili Yeye Bwana awe Bwana na mwokozi wa maisha yako.

(iv)Ujuzi ni jitiada za mtu mwenyewe,kipaji hutoka kwa Mungu,Karama utolewa na Roho mtakatifu kama apendavyo Yeye.

Kila aliyeokoka ana karama yake,kwa sababu sote tu viungo vya Kristo “Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.” 1 Wakorintho 12:7. Hivyo basi karama ;hutolewa na Roho mtakatifu kama apendavyo Yeye kwa wale watu wake wanaomcha.

Kumbuka;mtu wa mataifa asiyeamini hana karama,mpaka anapokuja kwa Bwana,akiokoka ndipo upewa karama moja wapo kwa kadri ya Roho mtakatifu apendavyo. Hata wewe mpendwa ipo karama yako ikiwa utakuwa ndani ya Yesu na Yesu awe ndani yako.

~Je mtu anaweza kuipata karama yake kwa kusomea darasani?

JIBU;

Karama haipatikani kwa kusomea darasani,kwa maana Yeye atoaye kila karama ni Roho mtakatifu.( 1 Wakorintho 12:8). Bali mwenye karama anaweza kwenda darasani kwa lengo la kuikuza karama yake kimaarifa ili atakapokua akiitumia aweze kuwa na wigo mkubwa wa matumizi ya karama hiyo.

Jambo hili leo limekuwa ni shida kubwa inayoisumbua kanisa la leo,maana wapo watu wanaohudumu kiroho huko makanisani kwa sababu walienda kusomea karama zao kisha baada ya mafunzo wengine wakajiita au kuitwa ni wachungaji,mashemasi,mitume,manabii N.K

pasipo Roho mtakatifu kuhusika kuwapa nyadhifa hizo. Mfano; Uchungaji hausomewi bali utolewa na Roho mtakatifu,kisha baada ya kupewa huduma hiyo mtu aweza kwenda shule kupata mwanga zaidi juu ya uchungaji alikadhalika na karama nyingine zozote zile.

Hatuwezi kuwa wachungaji,mitume,walimu kwa vyeti tu kwa sababu kinachohudumu kanisani sio cheti bali kile kinachohudumu ni roho ikiongozwa na Roho mtakatifu. Kama ndio hivyo,basi ni dhahili kabisa Roho mtakatifu ndie agawaye karama tofauti tofauti kama apendavyo Yeye.

~ Je mtu mmoja anaweza akawa na karama zote?

JIBU;

Mtu mmoja hawezi kuwa na karama zote,bali hupewa karama fulani kwa kufaidiana na mwingine ( 1 Wakorintho 12:14-20).

~Je mtu mmoja aweza kuwa na ujuzi wa jambo fulani,kisha akawa na kipaji na papo hapo akawa na karama?

JIBU; Ndio,mtu aweza akawa na ujuzi wa jambo fulani,akawa na kipaji kisha akawa na karama. Mfano mtu kabla ya kuokoka alikuwa na kipaji cha uimbaji wa nyimbo za kidunia,

then alipookoka ule uimbaji wake wa awali ukabadilishwa kwa Roho mtakatifu~ kile kipaji cha uimbaji kikavuviwa na Roho mtakatifu akawa na karama ya uimbaji,kisha mtu huyo akaonelea si vyema kubakia na karama hiyo pasipo kuijua kiundani hapo akaenda chuo cha mziki kwa ajili aikuze zaidi karama yake kwa ujuzi huku Roho mtakatifu naye akahusika kuikuza karama hiyo. Kwa hiyo umeona,mtu huyo amekuwa na ujuzi,kipaji pia karama.

~Je karama inahitajika kwa kiwango gani katika kanisa la leo?

JIBU;Karama inahitajika sana kwa kiwango cha juu katika kanisa la leo. Maana karama ndio utendaji kazi wa Roho mtakatifu,hivyo inahitajika. Kumbuka;mambo ya kanisa ni mambo ya kiroho na mambo ya rohoni huongozwa na Roho.

Hivyo basi ujuzi,kipaji na karama kila kimoja kinatofautiana na mwenzake haswa katika utendaji wa kazi. Tofauti hizi ndizo haswa zinazohitajika katika kanisa la leo ili makusudi mwili wa Kristo ujengwe.

02.TOFAUTI KATI YA WITO NA KARAMA.

Ipo tofauti iliyopo kati ya wito na karama,ingawa mara nyingine wito wa mtu inawezekana ndio ikawa ni karama yake.

A) Wito.(calling)

(i)Wito ni sauti kamili ya Roho mtakatifu juu ya kazi maalumu iliyotengwa kwa ajili ya yule aitwae. Mfano tunaona akina Barnaba na Sauli; “Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia.”Matendo 13:2

(ii) Wito ni kazi maalumu ya kiroho,au ofisi maalumu ya kiroho itolewayo na Roho mtakatifu kwa Yeye apendaye kumpa. Mfano katika zile huduma tano (Waefeso 4:11) ni wito uliotolewa na Roho mtakatifu,biblia inasema “Naye alitoa…” maana yake “ aliwafanya kuwa~ kwa wito.”

Tofauti iliyopo ni hii; mtu anaweza akaitwa awe mchungaji lakini katika uchungaji akapewa karama ya miujiza. Ndio maana waweza kuona wapo watu walioitwa kuwa wachungaji lakini wamejawa na matendo ya miujiza.

Kumbuk;wito huu ni uchungaji,bali karama katika uchungaji wake ni matendo ya miujiza. Mfano mwingine;mtu aweza kuitwa katika ofisi ya ualimu,lakini akapewa karama ya matendo ya huruma.

Ndio maana unaona walimu wengine makanisani wamejawa na matendo ya huruma sana. Mfano tena,mtu anaweza akitwa katika ofisi ya unabii lakini katika unabii wake akapewa karama ya kunena kwa lugha mbali na wito wa unabii.

Na mtu mwingine akawa na wito wa uinjilisti lakini akapewa ziada ya karama ya neno la maharifa,hivyo katika wito wake wa uinjilisti akawa amejawa na neno la maharifa. N.K


ITAENDELEA…

Kwa huduma ya maombezi tafadhali usisite kunipigia simu yangu hii;+255 655 11 11 49.

Mchungaji Gasper Madumla.

Beroya bible fellowship church(Kimara,Dar,TZ)

UBARIKIWE.

KWA TAARIFA YAKO: MPIGANAJI WA ISIS AAMUA KUOKOKA BAADA YA MUNGU WAKE KUTAKA KUMPELEKA JEHANAMU

$
0
0
Haya msomaji wetu wa Gospel Kitaa karibu katika kipengele chetu maalumu ''KWA TAARIFA YAKO'' ambacho kinakujia kila siku za alhamisi ndani ya GK kikiwa na lengo la kukupatia habari ambayo iliwahi kutukia lakini yawezekana huijui pia yawezekana ilitukia ukawa unaijua lakini GK ikawa imesahau mahali au kuna sehemu haina usahihi utapata fursa ya kusahihisha kwa kuweka comment yako chini kabisa kwenye habari husika. Karibu



KWA TAARIFA YAKO hapana shaka umeshasikia mengi kuhusu kile kinachoaminika na wengi kwamba waumini wa dini ya kiislamu ambao watapigana hadi kufa kutetea imani yao ikiwezekana hata kuua mtu hasa kumtetea mtume Muhamad basi moja kwa moja watakwenda peponi ambako watapumzika milele na kufaidi ahadi kedekede walizohaidiwa kwa mujibu wa imani yao (Hata hivyo sio waislamu wote wanaokubali hayo kwamba mtume aliagiza ukiua mtu kutetea uislamu utakwenda peponi). Basi KWA TAARIFA YAKO hii leo tunakutaarifu kuhusu na mmoja wa wapiganaji wa jihadi wa kundi lililojizoelea umaruufu sana la ISIS lililopo nchini Syria na Iraq ni kwamba mmoja wa wapiganaji wake aliamua kubadili dini na kumfuata Kristo mara baada ya kufika mbinguni na kutakiwa kwenda motoni kinyume na matarajio yake ya kuingia peponi.


KWA TAARIFA YAKO kwa mujibu wa taarifa zilizowahi kuandikwa na kutangazwa na Aleppo Herald ni kwamba mwanaume mwenye miaka 32 akiwa mpiganaji wa kundi la ISIS alijeruhiwa vibaya kwa risasi mpakani mashariki mwa Syria na kuachwa kufa hapo lakini mmoja kati ya wamisionari wa Kikristo kutoka eneo hilo alipomuona mtu huyo "akijua amekufa" alimua kumbeba ili akamzike Kikristo lakini baada ya kumbeba mtu huyo kwa mwendo wa kilometa kama 26 ndipo mtu huyo kimiujiza alipozinduka kutoka katika mauti ndipo mmisionari huyo alipoamua kutoa taarifa kwa kiongozi wake aitwaye Hermann Groschlin wote wakiwa katika kundi la Saint Dominican Catholic Presbytery of Ayyash masaa baada ya tukio hilo.


KWA TAARIFA YAKO kwa mujibu wa mtu huyo alisema mpiganaji huyo alimwambia mmishenari huyo kwamba kila siku alifundishwa kufia dini kutamfungulia geti la peponi, na alipokufa (mda masaa machache yaliyopita) alifika mbinguni ambako anasema wakati akielekea kwenye mwanga wa mbinguni ama peponi kama alivyosema mara akatokea shetani aliyemwelekeza njia ya kuzimuni ambako anasema aliweza kuona matatizo na uchangu aliowasababishia watu wengine sambamba na vifo alivyovisababisha kwa watu toka akiwa mdogo, ikiwa pamoja na kujionea namna alivyotenda kwa macho yake Kwa mujibu wa Groschlin amesema vitendo vya kijihadi alivyofanya mtu huyo vitaendelea kumuandama maishani maisha yake yote.


KWA TAARIFA YAKO mpiganaji huyo amedai kwamba kisha Allah ama Mungu kwa mujibu wake amesema alizungumza naye na kumwambia aliishi maisha mabaya sana na kwamba hataruhusiwa kuingia geti la mbinguni kama atachagua kufa, lakini endapo akitaka kuishi tena basi atakuwa na nafasi ya kutubu dhambi zake zote na kuishi njia njema za kumpendeza Mungu jambo ambalo alikubaliana nalo na ndipo aliporudishwa duniani na kuamua kuokoka na kuwa Mkristo siku chache baadae na kudai kwamba aliishi maisha ya kudanganywa awali kuhusu dini na imani yake kuhusu Mungu. Mpiganaji huyo ambaye pia inadaiwa majeraha yake yalipona haraka kuliko ilivyotarajiwa ameamua kujiunga na kikundi hicho cha Kikatoliki huku akimini kwamba habari yake itafanyika msaada kwa wapiganaji wa kundi la ISIS na kubadilisha njia zao na kumrudia Mungu wa kweli.

Hiyo ni KWA TAARIFA YAKO kama SPEISA ilivyoripoti, vinginevyo tukutane wiki ijayo....



NYOTA WA JOYOUS CELEBRATION AENDELEA KUSHANGAZA WENGI KWA UJASIRI WAKE

$
0
0
Sphumelele na mumewe katikati huku pembeni ni pastor Jabu kiongozi wa Joyous, siku ya harusi ya mwimbaji huyo
Aliyekuwa mwimbaji nyota wa kundi maarufu la Joyous Celebration la nchini Afrika ya kusini ambaye amemaliza mkataba wake mwanzoni mwa mwaka jana Sphumelele Mbambo ameendelea kuwashangaza mashabiki, rafiki na ndugu zake wanaomfuatilia katika ukurasa wake wa Facebook baada ya mwanadada huyo kumtakia heri ya kuzaliwa aliyekuwa mumewe wa ndoa anayedaiwa kumtelekeza mwimbaji huyo bila chanzo kujulikana.

Katika ukurasa wake mwimbaji huyo amemtakia heri mumewe huyo na kumsukumia injili kwa kumwambia Yesu anampenda. Unaweza kujisomea hapo chini

Happy birthday to My X-Husband Sakhile AKA Dj Kiteng God be with you in everything don't forget Jesus  is with you and He love's you unconditionally and He have Good plans for your live just praise Him and Celebrate the Gift of life I will always Pray and respect you as a person now you like a Brother to me enjoy the rest of your day to the fullest stay blessed and prepare your self for a brighter future and be ready for blessings that God have for you and don't forget that you are a Man nomatter what is happening in your life but nothing can take away the authority that God give you as a Man. after all the truth is we are all Children of God that keep us on the same side of life happy birthday




Sphumelele aliyetamba na nyimbo za kitamaduni tangu ajiunge na Joyous, alivunja ukimya kupitia ukurasa wake huo wa Facebook mapema mwaka jana pale alipoamua kuuambia umma kwamba amekimbiwa na mumewe kupitia salamu zake za kuzaliwa kwa mumewe huyo na kwamba hajajua hasa kisa cha kukimbiwa lakini alisema ameandika hivyo ili kumtakia amani na mafanikio huko aendako na angependa waendelee kuwa marafiki (kusoma habari hii bonyeza hapa). 



WAIMBAJI WAENDELEA KUMPA SALAMU BAHATI BUKUKU

$
0
0
Sehemu ya waimbaji kwenye msiba wa baba yake Bahati mwaka 2013. (Habari)
Waimbaji mbalimbali wa nyimbo za injili wamemtumia salamu za rambirambi muimbaji mwenzao Bahati Bukuku kufuatia kifo cha mama yake mzazi.

Mmoja kati ya waimbaji hao ni Ambwene Mwasongwe ambaye ametuma salamu hizo kwa njia ya whatsapp baada ya kuweka Profile picha ya Bahati Bukuku na kuandika ujumbe wenye maneno " Mungu akutie nguvu dada! Pole kwa kumpoteza mama"

Muimbaji mwingine ni Bupe Mizeck ambaye ameweke picha kwa whatsapp ambayo wamepiga pamoja na Bahati Bukuku na kuandika "Pole sana Rafiki yangu Bahati Bukuku kwa kufiwa na mama yetu mpenzi mrs Bukuku!! R I P mama!"

Mwaka 2013, Bahati Bukuku alifiwa na baba yake, Mzee Lwaga Bukuku, ambapo waimbaji kadha wa kadha pia walijitokeza kumfariji. (bofya hapa kuona)

Bahati Bukuku ni muimbaji wa siku nyingi wa nyimbo za injli nchini, ambaye amewahi pia kunusurika kifo kwenye ajali ya gari. (bofya hapa kuona)

NI ZAMU YA DVD YA DINA MGOMERA 17 JANUARI NDANI YA TAG ILALA

$
0
0
Kati ya mamvo ambayo yalikuwa yakisubiriwa mwanzoni mwa mwaka huu, basi ni tukio la tarehe 17 Januari, siku ambayo muimbaji wa nyimbo za injili, Dina Mgomera, atakuwa akizindua DVD yake ya Nina Haja Nawe.

Tukio hilo ambalo litasindikizwa na waimbaji kadha wa kadha ambao wataimba live, litafanyika kwenye kanisa la Tanzania Assemblies of God, Ilala. Baadhi ya waimbaji watakaokuwepo ni pamoja na wanaotoka One Voice Family International, Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, na wengineo wengi.

Mtazame Dina mwenyewe akizungumzia tukio hilo ambalo limedhaminiwa na kampuni ya Great Quality na Gospel Kitaa.



Unaweza pia kutazama video rasmi hapa chini;


Tukutane Jumapili ya tarehe 17 Januari ndani ya T.A.G Ilala, Gospel Kitaa itakuwepo kukuletea matukio yote.
Viewing all 1245 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>