Quantcast
Channel: Gospel Kitaa™
Viewing all articles
Browse latest Browse all 1245

HIVI PUNDE: JOYOUS 21 KUREKODIWA MAREKANI KWA T.D JAKES

$
0
0
Sehemu ya wapigaji Joyous20 Jijini Durban, ambayo GK ilihudhuria. (Picha zaidi)
Habari za hivi punde ambazo zimeifikia Gospel Kitaa zinaeleza kwamba ni rasmi albamu ya 21 ya kundi la Joyous Celebration itarekodiwa Potters House, kanisa linaloongozwa na Askofu T.D Jakes, lililopo Dallas.
Askofu Jakes akivunja ukimywa kwa waumini wake kuhusiana na ujio wa Joyous Celebration, na hapa akiwafafanulia waumini wake kwamba ni kama vile Beyoncé akubalikavyo nchini Marekani. Katika kuleta ulinganisho.


Habari hizi ambazo zimethibitishwa kwenye ibada ya leo nchini Marekani, ambapo Askofu Jakes ameeleza kwamba kundi hilo litafany alive recording kwa kushirikiana na kwaya wenyeji ya kanisa hilo.

Habari hizi zilizo njema kwa wadau wa muziki wa injili mahala pengi duniani hazijapokelewa vizuri na kila mtu, kwani baadhi ya mashabiki wameonyesha kusikitika na kwamba hali hiyo itawanyima fursa ya kuhudhuria tamasha hilo kwa kuwa ni gharama kusafiri, na lisha ya hivyo inaweza kupelekea nyimbo nyingi kuwa za Kiingereza badala ya lugha ya nyumbani.


BREAKING NEWS Bishop TD Jakes announces at his Sunday morning service in Dallas Texas that Joyous Celebration will...
Posted by MY Joyous Celebration on Sunday, 17 July 2016




Pamoja na waliolalamika, bado wengine wamefurahia zaidi na kuitaka Joyous ifike mbali zaidi katika kuhubiri injili kwa mataifa. Endelea kufuatilia GK nasi tutakufahamisha zaidi kuhusiana na habari hizi.


Viewing all articles
Browse latest Browse all 1245

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>